Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, April 2, 2010

USA Yafikiria Kutuma Ndege Za kivita Kusaidia Serikali Ya Somalia

Marekani inafikiria kutuma ndege zake za kipelelezi zijulikanazo kama "drones" pamoja na vifaa vingine vya kivita nchini Somalia ili kuisaidia serikali ya nchi hiyo katika vita vyake na wapiganaji wa Al-Shabaab wanaosadikiwa kuwa na uhusiano na kundi la kigaidi la al-Qaeda.
Ndege hizi za drones huongozwa na marubani ambao hubakia ardhini; na pamoja na mafanikio yake makubwa katika vita vya Iraq, Afghanistan na Pakistan, mara nyingi pia zimekosea shabaha na kusababisha maafa makubwa kwa raia.
Inavyoonekana Wamarekani hawataki kupeleka wanajeshi wao katika uwanja wa mapambano huko Mogadishu. Pengine bado wanakumbuka kisa cha mwaka 1993 ambapo wanajeshi wake 18 waliuawa na hatimaye kuwafanya wafungashe virago kwa haraka haraka na kuondoka.
Naamini kwamba tatizo la Somalia ni letu Waafrika na kama kweli tungekuwa na nia ya dhati la kulitatua tungeweza

Rubani aliyeko ardhini akiwa anaendesha ndege hizo

No comments:

Post a Comment