Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, April 2, 2010

59 Wajitokeza Kumrithi Maximo

Makocha 59 Wameweza kujitokeza kutaka kurithi nafasi ya Kocha Marcio Maximo, ya kuinoa timu ya taifa ya soka 'Taifa Stars' na hayo yalisemwa na Shirikisho la soka Tanzania (TFF).Raisi wa TFF, Leodegar Tenga, alisema kuwa miongoni mwa maombi hayo 59 waliyopokea, makocha watatu ni wazalendo, na watatu wengine wanatoka nchi za Afrika ambazo ni Kenya, Cameroon na Ghana huku wengine wakitokea bara la Asia na wawili wakitokea Amerika ya Kusini.

Alisema kwamba makocha 48 waliobaki, wanatoka barani Ulaya na akaongeza kuwa wengi wao wana uzoefu na uwezo mkubwa wa kufundisha timu za taifa.

Mbali na hilo alisema walipokea ombi moja kutoka kwa kocha Mzalendo, ambaye aliomba nafasi ya kuwa kocha msaidizi lakini ombi lake limetolewa kwa sababu lengo ni kutafutwa kwa kocha mkuu.

Mpaka sasa mchakato wa kupitia maombi hayo na hatua waliyopo, ni kwamba baadhi wameandikiwa barua ya waombaji ya kutaka kufahamu sasa wanafanya nini.

Kwani wanahitaji walipwe kiasi gani cha mshahara, na muda gani ambao wanaweza kujiunga na Stars endapo watakuwa wamefikia makubaliano.

"Tumewaeleza kwamba watupe majibu kabla ya Aprili 15. Kwa ufupi tumefurahishwa na idadi kubwa ya maombi yaliyojitokeza safari hii ukilinganisha na ilivyokuwa huko nyuma, wakati ule tulipokea maombi 18 tu na kati ya hayo, 15 tuliwaomba kwa kuwabembeleza," alisema Tenga.

Aliongeza kwamba mchakato huo ni mgumu sana na wanaufanya kwa umakini ili waweze kupata kocha bora atakayeendeleza mafanikio yaliyopo hivi sasa.

Mbali na kuwa na sifa za ziada, shirikisho litatoa kipaumbele kwa kocha ambaye atakuwa na uzoefu wa kufundisha makocha wengine na mwenye cheti kinachotambulika kimataifa.

Alimalizia kwa kusema kwamba si vyema kutaja majina ya makocha walioomba, ili kulinda heshima na pia kuthamini maamuzi yao waliyoyafanya ya kuomba ajira hiyo.

EASTER TRAFFIC LIGHT PARTY


EASTER IS HERE!!... AND WE HERE TO MAKE SURE U GET THE BEST OUT OF IT...Y'LL KNOW WHERE IT ROCKS EVERY FRIDAY...ONLY NOW WE CODING HOW WE DO IT...

WE GO ALL OUT YET AGAIN TO GIVE U ANOTHER UNFORGETTABLE NITE....
PRESENTING U KUALA LUMPUR'S BIGGEST ★ ★EASTER TRAFFIC LIGHT PARTY★ ★

YOU all know the rules:

■ RED= No-go zone. In your Dreams!
■ YELLOW= It's complicated, but give it a try!!
■ GREEN= Single and Ready to Mingle!!!

THESE RULES ARE .NOT. OBLIGATORY BUT ARE ENCOURAGED....

LET COLOUR PLAY CUPID AND EXPRESS YOUR SINGLEDOM THROUGH THE ALL TIME CLASSIC TRAFFIC LIGHT PARTY..

For all you sexy ladies and handsome guys who are single and ready to mingle, this is your night !
LOOK OUT FOR PEOPLE WEARING GREEN !
YOU MIGHT JUST GET LUCKY !!

SPICIN UP THE PARTY ATMOSPHERE WIT CRAZY TUNES, LIVE DJs ( KLs FINest STeeL SPinnERs) WILL SPIN U WILD!!!.

LINE UP:

★DeeJAy SnipER

★DeeJaY ViNI

★DeeJay SLIm

★Roc BOy DeeJaYs

EXPECT THE "BOOM BOOM POW" FUSION.... HEAVY MUSIC !!!!

>LIVE PERFOMANCES AND A FASHION SHOW THAT WILL TAKE UR BREATH AWAY!!!

* FREE FOR ALL LADIES TILL 12:00 WITH FREE DRINKS AS WELL TILL 12:30...SO GET THERE ON TIME!!!!

★ NYAMA CHOMA,LOADS OF BEER,MSHIKAKI,KACHUMBARI WILL BE AVAILABE...

*SHISHA AVAILABLE ALL NITE LONG...


* DRESS CODE: IF NOT GOIN BY THE RULES THEN MAKE SURE U DRESS TO IMPRESS... STRICTLY NOT HATS, NO HOODS..

■ ■ ■ ENTRANCE

AFTER 12:00 GENTS RM 40
LADIIES RM 30

▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀▀
INFO,VIP & BIRTHDAY GROUP BOOKINGS

0173953930
0142303552

LETSSSS MAKEE THISSS ANOTHER NIGHT TO REMEMBERRRR!!!! MAXIMUM
FUN GUARANTEED!

C U THERE>>>>>>>>>


SECURITY WILL BE IN FULL EFFECT!!

Kamuzi La Flava Nite Kiafrika Zaidi @ Mzalendo Pub Pasaka hii

Tangazo La Msiba Wa Eveline Gembe


marehemu Eveline Gembe wakati wa uhai wake
Familia ya Bwana na Bibi Gembe wa Upanga-Dar-es-salaam na Tabora, wanasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Evaline Gembe(pichani) kilichotokea hapo juzi tarehe 30.3.2010 huko Toronto,Canada.Evelyne amefikwa na mauti katika hospitali ya St.Michael’s ya Toronto alipokuwa amelazwa.

Taratibu na mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda nyumbani Tanzania kwa mazishi zinafanyika nyumbani kwa dada yake, Julie huko huko Toronto,Canada.

Ukiwa kama mtanzania,ndugu,jamaa au rafiki, unaombwa kuchangia fedha,hali na mali kwa ajili ya kuwezesha kuusafirisha mwili wa marehemu kurudi nyumbani kwa mazishi mapema kadri iwezekanavyo kwani kama wengi wenu mnavyofahamu, mwili unavyozidi kukaa Funeral-Home,gharama ndivyo zinavyozidi kuongezeka. Mwili utasafirishwa punde tu zitakapopatikana fedha za kutosha kwa ajili ya kulipia gharama husika.

Unaweza kutuma mchango wako kwenye Account maalumu ya wafiwa kama ifuatavyo:

BANK : CIBC (Canadian Imperial Bank of Commerce)

ACCOUNT NUMBER: 5681839
TRANSIT NUMBER: 00902
INSTITUTE NUMBER: 010
SWIFT CODE: CIBCCATT

Vilevile unaweza kutumia E-mail Money Transfer kwa Sania Esmail.Anuani yake ni saniae@yahoo. ca au kuwakilisha msaada wako kwa kutumia anuani hii:

1025 SCARLETT ROAD, APT 606, BUZZ # 178
TORONTO ON, M9P 3V3.
Kwa mawasiliano zaidi unaweza kuwasiliana na wafuatao:

Julie +1 416-247-8318
Esmail Manambi- +1 647- 299-2572
Victor Wambura- +1 647-428-4118
Prosper Luteganya- +1 905 626 3764

Tafadhali chukua muda kuwafariji na kuwaombea ndugu,jamaa na marafiki waliofikwa na msiba huu. Tunatanguliza shukrani kwa misaada yote iliyotolewa na itakayotolewa. Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi.

- Amen.

Makamanda Kibao Wa Wa Jeshi Polisi Nchini Wapandishwa Vyeo

Na Mohammed Mhina
na
Athumani Mtasha

wa Jeshi la PolisiRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama nchini Mh. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, amewapandisha vyeo maafisa 42 wa Jeshi la Polisi kutokana na utendaji wao mzuri wa kazi.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msaidizi Abdallah Mssika, imesema kuwa waliopandishwa vyeo kuanzia Machi 16, mwaka huu ni pamoja na Makamanda wa Polisi wa mikoa tisa, Makamanda watano wa vikosi na Wakuu wa Vitengo mbalimbali vya Jeshi hilo waliopo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Dar es Salaam na Zanzibar.

Kamanda Mssika amesema kati ya hao wapo Maafisa wanne wakuu ambao wamepandishwa vyeo kutoka vyeo vyao vya zamani vya Makamishna Wsaidizi Wandamizi wa Polisi (SACP) na kuwa Manaibu Makamishna wa Polisi (DCP).

Waliopandishwa kuwa Manaibu Kakamishna wa Polisi (DCP’s) ni Mkuu wa Huduma za Polisi Jamii Makao Makuu ya Jeshi la Polisi SACP Isaya Mngulu, Kamanda wa Polisi Kikosi cha Afya nchini SACP Neven Mashayo, SACP Rashid Omari Ali, wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam SACPO Suleiman Kova.

Kamanda Mssika amewataja Makamanda 38 wakiwemo Makamanda wa Polisi wa Mikoa tisa ya Tanzania Bara na Visiwani kutoka Vyeo vya Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP ambao sasa kila mmoja anakuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) ambao ni Makamanda Thobias Andengenye wa Morogoro, Henry Salewi wa Kagera, Bi Celina Kaluba wa Singida na Kamanda Lucas Ng’hoboko wa Kilimanjaro.

Wengine ni Kamanda Absalom Mwanyoma wa Pwani, Simon Sirro wa Mwanza, Isuto Mantage wa Rukwa, Michael Kamhanda wa Ruvuma na Yahaya Rashidi wa mkoa wa Kaskazini Pemba.

Kamanda Mssika amewataja Makamanda wa Vikosi waliopandishwa vyeo kuwa ni Mohammed Mpinga, wa Kikosi cha Usalama Barabarani Tanzania, Kamanda Tresphory Anaclet wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia nchini (FFU), Sospeter Kondela, Kamanda wa Polisi Kikosi cha Ujenzi, Geofrey Nzoa Kamanda wa Polisi Kitengo cha Kuzuia na kupambana na Madawa ya Kulevya na Mkuu wa Chuo cha Polisi cha Dar es Salaam Bi. Alice Mapunda.

Wengine ni Mkuu wa Shirikisho la Polisi wa Kimataifa Interpol hapa nchini Kamanda Hussein Nassoro Laizer, Mkuu wa Bohari Kuu la Polisi nchini Kamanda Adriano Magayane, Mkuu wa Kikosi cha Usafirishaji cha Jeshi la Polisi nchini Kamanda Kamanda Ali Mlege na Mkuu wa Kitengo cha Fedha cha Jeshi la Polisi nchini Kamanda Jonas Mgendi.

Wengine ni Mwakilishi wa Jeshi la Polisi Tanzania kwenye Ofisi za Interpol Kanda ya nchi za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika Kamanda Goodluck Mongi, Mkuu wa Kitengo cha Picha na Maabala ya Uchunguzi wa Vielelezo vya Makosa ya Jinai nchini (FB) Kamanda Hezron Gyimbi.

Wengine ni Kamanda Jamal Rwambow, Kamanda Lucas Haule na Kamanda Donald Ludamila wa Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Makao Makuu, Mkuu wa Kitengo cha Maboresho cha Jeshi la Polisi nchini Kamanda Lucas Kusima, Kamanda Saidi Juma Hamis kutoka Ofisi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Makao Makuu.

Kamanda Mssika amesema kuwa wengine walipandishwa ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mifumo ya Mitangao ya Kompyuta ya Jeshi la Polisi nchini kamanda Anyisile Kyoso, Kamanda Renatus Chalamila, Mwanasheria wa Jeshi la Polisi nchini Kamanda Donald Kaswende na Kamanda mwanamke Adolfina Chialo.

Wengine ni Mkuu wa Kitengo cha Mafunzo cha Jeshi la Polisi nchini Kamanda Abdulrahman Kaniki, Msaidizi wa Mkuu wa Operesheni Maalum nchini Kamanda Hezron Kigondo, Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zananzibar Kamanda Mussa Alli Mussa na Kamanda Hamdani Makame wa Ofisi ya Kamishna wa Polisi Zanzibar.

Mkuu wa Mipango Kamanda Ernest Mangu, Kamanda Makame Ali Makame, Kamanda Mwalim Ame na Kamanda Mpinga Gyumi ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Malalamiko Makao Makuu ya Jeshi la Polisi.

HIA ENDI ZEA!

Dj JD, Dj Juicy, na Dj Q kuwasha moto Kigamboni Pasaka hii


Kwa mara nyingine wakazi wa Kigamboni watapata burudani katika siku tatu za Pasaka ambayo inaratibiwa na Club ya Chadibwa.Burudani hiyo ambayo inajumuisha disco la kila jumamosi, ambapo kutokana na sikukuu yenyewe uongozi umeamua kuongeza siku ya Jumapili na Jumatatu.



Akizungumza mmoja wa viongozi wa Klabu hiyo Robert Mwafrika amesema kuwa wameamua kuwaletea burudani wakazi wa Kigamboni ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakivuta kufuata burudani upande wapili.




"Tumeamua kuwaletea burudani ambayo kwa sasa ni Disco pekee linapigwa Beach kabisa huku kukiwa na ulinzi wa kutosha na Disco lenyewe linaletwa na Ma Dj wenye uzoefu, DJ John Dilinga aka Everlasting Dj JD, akishirikiana na DJ machahari kwenye machine DJ Q pamoja na DJ Juicy ambao kwa pamoja huwa wanafanya usiku kuonekana mfupi" alisema Mwafrika.

Aidha akifafanua Robert amesema kuwa siku ya Jumapili kutakuwa na Disco Toto kuanzia saa nne asubuhi hadi saa 12 jioni kabla ya kuanza Disco la watu wazima kuanzia saa tatu usiku.


Kama hiyo haitoshi mambo ya vilaji na vinywaji uongozi umehakikisha watu wataburudika vyakutosha.Chadibwa ikishirikiana na Fire Burn Disco Theque walianza kupiga muziki wiki iliyopita ambapo inasemwa ilikuwa na mafanikio na muitikio mzuri sana na Disco hili litakuwa ni la kudumu kila Jumamosi ambapo mashabiki watapata burudani