Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, September 29, 2010

Muswada wa Obama wa kudhibitiwa Internet nchini Marekani


Rais Barack Obama wa Marekani anajiandaa kuwasilisha muswada wa kudhibitiwa matumizi ya Intaneti nchini humo.
Kwa mujibu wa muswada huo, maelezo binafsi ya watumiaji wa Intaneti ikiwa ni pamoja na barua-pepe zao na mitandao ya kijamii zitakuwa zinawafikia moja kwa moja polisi wa FBI.

Gazeti la New York Times limeripoti habari hiyo na kuongeza kuwa, kama muswada huo utapitishwa, basi maelezo ya wanachama wa mitandao ya kijamii kama vile Facebook na Skype yatakuwa yanawafikia moja kwa moja polisi wa Marekani FBI itakapobidi.
Muswada huo unatarajiwa kuwasilishwa mbele ya Baraza la Congress la Marekani mwaka ujao wa 2011.

Maafisa usalama wa Marekani wanasema kuwa inabidi sheria na hatua mpya zichukuliwe kwa ajili ya kudhibiti na kuwekea mipaka matumizi na mawasiliano ya Intaneti nchini humo.
Lakini baadhi ya weledi wa mambo wameelezea wasiwasi wao kuwa hatua hizo mpya zitapelekea watu wenye nia mbaya kupenya ndani ya barua-pepe za watu binafsi na kufanya uhalifu na uharibifu.

Haramia wa kisomali akamatwa Tanzania


Jeshi la Tanzania limesema limemkamata mshukiwa mmoja wa Uharamia raia Somalia, kufuatia makabiliano makali ya ufyatulianaji wa risasi katika bahari ya Hindi.

Ripoti zinasema tukio hilo lilitokea siku ya Jumapili iliyopita katika eneo la Kusini mwa pwani ya Tanzania, eneo ambalo meli ya kampuni ya kuchimba mafuta ya Ophir inafanya utafiti ili kubainisha ikiwa eneo hilo lina utajiri wa mafuta ya Petroli.

Msemaji wa jeshi la wanamaji nchini Tanzania, Steve Buyuya, amesema manuawari ya kijeshi ilishambuliwa kwa risasi na maharamia waliokuwa kwenye mashua ndogo.
Lakini baada ya ufyatulianaji wa risasi uliodumu kwa muda, maharamia kadhaa walifanikiwa kutoroka huku mmoja wao akikamatwa na wanamaji wake.

Andrew Chenge akamatwe haraka- Mahakama Yatoa Amri




BAADA ya kutoonekana mahakamani jana , Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kinondoni, Dar es Salaam imeamuru kukamatwa kwa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge.
Chenge ambaye yuko nje kwa dhamana akikabiliwa na mashitaka ya kusababisha vifo vya watu wawili, jana hakufika mahakamani hapo wala mdhamini wake bila taarifa.
Amri hiyo ilitolewa mahakamani hapo na Hakimu Sundi Fimbo, baada ya mwendesha mashitaka, Richard Rweyongeza kusoma maelezo ya awali ya mashitaka yanayomkabili mshitakiwa.

“Haijalishi kuwa mshitakiwa yuko kwenye kampeni au wapi, Mahakama haitambui jambo lolote kuhusu kampeni, hivyo kwa kuwa hajahudhuria mahali hapa, inabidi akamatwe kwa kushindwa kutekeleza amri ya Mahakama,” alisema Hakimu Fimbo.
Alifikia uamuzi huo baada ya masharti ya dhamana ambayo yanamtaka mshitakiwa kufika mahakamani siku ya kesi aliyopangiwa na bila hivyo atoe taarifa za kutofika kwake mahakamani.

Kwa niaba ya Hakimu Mkazi, Kwey Rusema, ambaye anasikiliza kesi hiyo, Hakimu Fimbo aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 5 mwaka huu itakaposikilizwa tena.
Ilidaiwa kuwa Machi 27, 2007 mshitakiwa akiendesha gari aina ya Toyota Hilux namba T 512 ACE alimgonga mwendesha pikipiki ya magurudumu matatu - bajaj jijini Dar es Salaam na kusababisha vifo vya Beatrice Costantine na Victoria George.
Awali baada ya Mahakama kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka, Mahakama ilisema Chenge ana kesi ya kujibu na alitakiwa kufika mahakamani jana kuanza kusikiliza utetezi wake.

Chenge ambaye anatetea ubunge Bariadi Magharibi alisema ataleta mashahidi wawili ambao ni yeye na shahidi mwingine ambaye hakutajwa mahakamani.
Aidha, katika kesi hiyo shahidi wa mwisho wa upande wa mashitaka, Raymond Njeje, alidai kuwa stika ya bima aliyokuwa akitumia Chenge si mali yake.
Njeje alidai kuwa, stika hiyo ni ya gari namba T 571 AKH aina ya Toyota RAV4 nyeusi na si ya Toyota Hilux iliyosajiliwa kwa namba T 513 ACE ambalo alikuwa akiendesha Chenge wakati anapata ajali.

Alidai stika hiyo namba 11919156 inamilikiwa na Evarist Ses iliyotolewa mwaka 2007 kwa ajili ya matumizi ya miezi mitatu kuanzia Juni 29 hadi Septemba 28.

Monday, September 27, 2010

Titus Bramble atuhumiwa kubaka!!


Mlinzi wa timu ya Sunderland Titus Bramble, amekamatwa baada ya mwanamke kubakwa kwenye hoteli moja mjini Newcastle.

Mchezaji huyo wa Ligi Kuu ya England amekamatwa pamoja na mtu mwengine katika hoteli ya Vermont mapema siku ya Jumatano na wanahojiwa na polisi.
Bramble mwenye umri wa miaka 29 amekamatwa kwa kushukiwa amebaka baada ya polisi kupigiwa simu na mwanamke mmoja.

Klabu ya Sunderland hadi sasa haijazungumza lolote kuhusiana na tuhuma hizo. Bramble alijiunga na klabu hiyo akitokea Wigan msimu huu.

Mwanamke mwenye matatizo ya akili anyongwa Marekani.


Teresa Lewis mwanamke mwenye umri wa miaka 41 mwenye matatizo ya akili amenyongwa leo nchini Marekani kwenye jimbo la Virginia, kwa kosa la kumuua mumewe na mjukuu wake wa Kambo.

Teresa ni mwanamke wa kwanza kuhukumiwa adhabu ya kifo nchini Marekani tangu mwaka 1912 na amesubiri kutekelezewa adhabu hiyo kwa muda wa miaka mitano.
Mwanamke huyo ameuawa kwa kudungwa sindano ya sumu. Maswali mengi yamejitokeza kuhusiana na uwezekano wa mama huyo aliyekuwa na kiwango cha akili cha IQ 72 kupanga na kutekeleza mauaji hayo ya watu wawili, ambaye pia imejulikana alikuwa na matatizo ya akili.

Mahakama kuu ya Marekani na Gavana wa jimbo la Virginia walikataa kuondoa adhabu hiyo ingawa wengi wametilia shaka kesi hiyo na maelfu ya watu walitaka iondolewe. Virginia ni jimbo la pili nchini Marekani linaloongoza katika utendaji vitendo vya jinai.

TAKUKURU yamsafisha Waziri Batilda Buriani!


TAASISI na Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha imekenusha kuwashikiliwa baadhi ya wafuasi wa mgombea ubunge wa Arusha Mjini, Dk. Batilda Burian, ambao pia ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa tuhuma za kuhusishwa na rushwa katika uchaguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana mkoani hapa, Kamanda wa taasisi hiyo Mkoa wa Arusha, Ayubu Akida, alisema habari hizo zimetolewa pasipo kufanyiwa uchunguzi wa kina.

Kamanda Akida alisema ni kweli walipata taarifa ya kuwepo kwa kikao katika nyumba moja katika Kata ya Baraa jijini hapa, ambapo washiriki hao wangegawiwa fedha ili kuwashawishi wapiga kura kumpigia kura mgombea ubunge wa Arusha Mjini ambaye ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dk. Burian.

Alibainisha kuwa maofisa wa Takukuru walifika katika nyumba hiyo jioni na kujichanganya na watu waliokuwamo ndani ya nyumba hiyo ambao baadaye walibainika kuwa wanavikundi na wanachama wa CCM waliokuwa na vikao vya ndani lakini hakukuwapo na tukio la utoaji wa fedha.

Alisema baada ya kubaini hilo maofisa wa Takukuru hawakuona sababu ya kuwakamata wanachama hao kwa kuwa CCM wana utaratibu wa kuwa na vikao vya ndani, ambavyo wao huviita kampeni za nyumba kwa nyumba ambapo mgombea hukutanishwa na wananchi ili kueleza sera zake.

“Unajua haya yanayosemwa ni njama za kunichafua kisiasa zaidi mbele ya wapiga kura ambao hata saa nane za usiku wapo tayari kuichagua CCM… mwanzo nilizushiwa kuhusu ndoa yangu, sasa wameona wakimbilie TAKUKURU na kunichafua katika vyombo vya habari, mimi ni mkomavu wa kisiasa, sina wasiwasi na haya,” alisema Dk. Batilda.

Madini yaliingizia Taifa Trilioni 5!!


SEKTA ya madini nchini imeingiza kiasi cha sh trilioni tano, kwa kipindi cha miaka mitano ya utawala wa Awamu ya Nne, lakini kiasi hicho cha fedha hakijaweza kukidhi bajeti ya elimu iliyofikia zaidi ya sh trilioni nane.

Takwimu hizo zilitolewa juzi na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alipokuwa akiwahutubia wananchi waliofika kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za ubunge wa CCM Jimbo la Buchosa, wilayani Sengerema, mkoani Mwanza, zilizofanyika Kata ya Nyakarilo -Buchosa.

Waziri Ngeleja alisema kiasi hicho cha fedha kimetumika kwenye huduma mbalimbali za maendeleo ya taifa na wananchi wake na kamwe si rahisi kwa chama au mgombea kuahidi na kutekeleza ahadi ya kutoa elimu bure.

Alisema pamoja na baadhi ya wagombea kujinasibu kuwa wana uwezo wa kutoa elimu ya bure kwa kutegemea mapato yatokanayo na sekta ya madini jambo hilo haliwezekani kwa sababu kinachopatikana ni kidogo kulinganisha na mahitaji.

“Wananchi msije mkapotoshwa na ahadi hizi za wagombea kutoka upinzani eti watatoa elimu bure kwa fedha za madini…hiyo haiwezekani hata kidogo, mwaka 2005 hadi mwaka huu 2010, sekta ya madini hapa nchini imeingizia serikali sh trilioni tano, zitatoshaje kwenye sekta ya elimu?” alihoji.

Waziri Ngeleja alibainisha kuwa mataifa tajiri duniani yanayoendesha migodi kwa miaka mingi, ikiwamo Marekani, hakuna wawekezaji wanaolipa kodi zaidi ya asilimia 50 ya pato la uzalishaji unaopatikana.

Aliongeza kuwa utekelezaji wa miradi yote ya maendeleo katika sekta zote hutegemea bajeti ya serikali, hivyo mtu binafsi hawezi kusema atatekeleza ahadi zake bila kupitia mipango ya serikali yenyewe.

Wateja wa Vodacom kuchati bure kwa Intaneti


Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom Tanzania, imezindua huduma mpya ya Intaneti ambayo itawawezesha wateja wake kuchati kwa intaneti bure.

Mkurugenzi wa Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Bi Mwamvita Makamba alisema jana kwamba wateja wa Vodacom sasa wanaweza kuchati bure kwenye tovuti za Face Book, the Grid na Vodamail.

Alisema Vodacom Tanzania inatoa huduma hiyo kwa lengo la kuwawezesha wateja wake kupata muda wa kuchati zaidi.

Alifafanua kwamba hayo yote yatawezekana kwa kutumia mtandao wa 3G ambao una kasi na nguvu kubwa.

“Tunapenda wateja wetu watumie mtandao wetu kwa kuwasiliana bure na hivyo kukata kiu yao ya mawasiliano”.

Alitoa wito kwa wateja wa Vodacom na Watanzania kwa ujumla kutumia huduma hiyo ya mtandao wa Intaneti.

Aliwaomba Watanzania kujiunga na Vodacom ili kupata huduma hiyo bure na hivyo kuwasiliana zaidi.

Alisema huduma hiyo itapatikana kwa simu za mkononi na pia kwa Laptop zilizounganishwa na USB Moderm.

Thursday, September 23, 2010

Ban Ki Moon Amteua Mkapa Kuongoza Jopo Sudan Kusini


Mwandishi Maalum

New York- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon amemteua Rais
Mstaafu wa Tanzania Benjamin William Mkapa ,kuongoza jopo la tume ya watu
watatu itakayoangalia mchakato wa kura za maoni Sudan Kusini na Jimbo la
Abyei.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Umoja wa Mataifa ( jana jumatano),
uteuzi huo unatokana na maombi yaliyotolewa pande mbili zinazounga mkono
makubaliano ya amani ya kudumu nchini Sudan.Pande hizo ni Serikali ya Sudan
na Kikundi cha People’s Liberation Movement.

Wengine walioteuliwa ni aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Ureno,
Bw. Antonio Moteiro na Bw. Bhojraji Pokharel Mwenyekiti wa zamani wa Tume
ya Uchaguzi nchini Nepal.

Akizungumzia uteuzi huo, Ban Ki Moon anasema ana imani kwamba tume
aliyoiteua itasaidia kufanyika kwa kura hiyo ya maoni itakayozingatia matakwa
ya watu wa Sudan Kusini na Jimbo la Abyei

Jukumu kubwa la tume hiyo pamoja na mambo mengine ni kufanya ziara za mara
kwa mara nchini Sudani katika kipindi chote cha mchakato wa kuelekea kura za
maoni. Upigaji wa kura za maoni unatarajiwa kufanyia mwezi Januari 2011

Tume hiyo pia inatarajiwa kukutana na kushirikiana na pande zote zinazohusika
katika mkataba wa amani, tume inayoratibu kura ya maoni, jumuia za kiraia na
makundi ya waangalizi wa kura hiyo.

Pamoja na kutoa taarifa kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, tume hiyo
itafuatilia kwa karibu mchakao mzima wa kura za maoni na pia masuala ya
kisiasa na hali ya usalama.

Tume itatakiwa pia kufanya kazi ya kuhakikisha inaimarisha imani ya mchako
wa kura za maoni, kuhakikisha na kuzitaka pande husika na viongozi kuchukua
hatua za pamoja za kutatua matatizo yoyote au migogoro itakayojitokeza.

Wananchi wa Sudan Kusini watapiga kura yao ya maoni kuamua iwapo wajitenge
na Serikali ya Khartoum ,wakati wananchi wa Jimbo la Abyei linalogombaniwa
na pande zote mbili ,wao watapiga kura ya kuamua wajiunge na upande upi
iwapo Sudan Kusini itajitenga na Kaskazini.

Upigaji wa kura ya maoni ni miongoni wa mabadiliko yaliyofikiwa katika Mkataba
wa Amani wa mwaka 2005(CPA), uliomaliza vita vya zaidi ya miongo miwili nchini
humo. Aidha kura hiyo ni muhimu sana kwa mstakabali wa nchi yote ya Sudan.

Swebe ainyemelea siasi

Unamkumbuka toto tundu Swebe, yule aliyekuwa akiigiza enzi zile na kina Kipemba, Bi Staa, Kibakuli, Mhogo Mchungu, Kingwendu, Bi Hindu, Sandra, Nina, Nora na wengine wengi?Adam Melele ndiyo jina lake halisi.

Mara ya mwisho alionekana kwenye maigizo ya kundi la Kaole Sanaa Group mwaka 2004 na tangu wakati huo amekuwa akionekana kwenye filamu mara moja moja tofauti na wasanii wenzake kama Ray, Kanumba, Johari na wengine ambao huonekana katika filamu mpya kila kukicha.

Swebe amezungumza na kueleza sababu zilizomfanya asiuze sura mara kwa mara kama wafanyavyo wakongwe wenzake.


"Hivi sasa nafanya kazi za kijamii, niliajiriwa katika kampuni ya Experimental Marketing kama mhamasishaji juu ya ugonjwa wa Ukimwi kwa vijana, sikuweza kupata muda wa kufanya kazi ya sanaa ingawa pia nilikuwa nikiifurahia hii kazi ya uhamasishaji kutokana na ukweli kwamba vijana wenzetu wengi wamemalizwa na gonjwa hili" alisema.

Msanii huyo alisema baada ya kufanya kazi hiyo kwa miaka kadhaa sasa ameamua kurudi kwenye sanaa na sasa amekuja kuwasaidia wasanii wachanga kwa kuandaa shindano la IBUA Film Star Tanzania.

" Unapozungumzia sanaa ya maigizo nchini unakuwa kama unawazungumzia watu fulani tu ambao wamelishikilia soko hili, mimi nimekaa pembeni na kuona kuwa kwa mtindo huu soko letu halitakuwa tunahitaji kuwa na damu changa itakayochangamsha soko,

Ipo siku wateja wetu watachoka kwa kuwa watu ni wale wale na vitu vinavyozungumziwa kwenye filamu ni vile vile, tunawahitaji watu wengine watakaoleta changamoto mpya kwenye soko hili" alisema .

Swebe alisema yeye kama muasisi wa shindano la IBUA na mkongwe wa sanaa ya maigizo nchini anaamini watu wachache hawawezi kuleta mabadiliko lakini uzoefu wao utaendelea kutumika siku zote.

"Kwa kutumia uzoefu wangu nimeanzisha shindano hili lakini nahitaji mawazo ya wakongwe wenzangu ili tufanikishe zoezi hili kwa kuwa litatunufaisha wote, soko la filamu Tanzania likikua sitafanikiwa peke yangu bali wote tuliomo kwenye jahazi hili" alisema.

Wakati akiendelea na mikakati ya kuipeleka sanaa ya filamu mbele, Swebe pia amejiingiza kwenye siasa, alipokuwa anatema cheche alikuwa mbioni kuelekea kwenye kampeni huko Magomeni ambapo anagombea Ujumbe wa Serikali za Mitaa katika mtaaa wa Idrisa.


alipokuwa jaji kwenye IBUA Film Star
"Nikimalizana na wewe naelekea kwenye kampeni, nataka kuwatumikia wananchi wangu ambao kwa kweli wamekuwa wakiniunga mkono sana kwenye sanaa, sasa umefika wakati wa kuwalipa fadhila kwa kuwasimamia na kuwatetea iwapo nitachaguliwa hapo kesho" alisema Swebe.

Miaka miwili iliyopita Swebe alikuwa akionekana na kundi la Wanaume Family wakati ule halijagawanyika, akizungumzia uwepo wake kundini humo alisema ilikuwa na lengo la kuwapa kampani washkaji zake.

"Mimi sio muimbaji nilikuwa nao kama marafiki ambao tulikuwa tukishauriana mambo mengi, lakini sasa nimetingwa na shughuli nyingine nyingi ndio maana sionekani tena kwenye kambi hizo ambazo sasa zinekuwa mbili" alisema.

Kila la kheri Swebe

Neno La Leo: Degedege Si Ugonjwa Wa Watoto Tu


Na Maggid Mjengwa,
KWA kawaida degedege ni ugonjwa wa watoto. Dalili zake ni mtoto kupandwa na homa na mwili kutetemeka . Ni ugonjwa wa hatari sana. Utotoni tuliamini, kuwa ukiugua degedege, basi, hutaugua tena ukubwani.

Kumbe, kuna degedege la ukubwani pia, hususan kwenye masuala ya siasa na kampeni za uchaguzi kama hizi za sasa. Nilipata kuandika, kuwa siku hizi kila asubuhi ni burudani kusoma baadhi ya vichwa vya habari magazetini au kuangalia habari za kwenye runinga na kusikiliza redio. Kila kukicha kuna kituko kipya Afrika, ilipatwa kusemwa

Chini Ya Ulinzi



Operesheni ya kuwakamata wapiga debe Manispaa ya Morogoro hivi karibuni

!Mzee Wa Libeneke Akiwa Iringa


Michuzi (katikati) akiwa na kamanda wa FFU mkoa wa Iringa Said Mnunka( kushoto) na kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa (ACP) Evarist Mangalla ,Michuzi amekutana na makamanda hawa leo nyumbani kwa aliyekuwa mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa mzee Tasili Mgoda. (Picha: Francis Godwin, Iringa.)

HOT NEWS FROM BIG BROTHER All Stars.


Meryl and Mwisho both agree that Mwisho is more nervous about Saturday's engagement than Mery

Wanasiasa waongo, wanaichezea Mahakama

MAJAJI na mahakimu wamekiri kutofahamu kabisa sheria za uchaguzi hivyo kusababisha baadhi ya wanasiasa kuzichezea mahakama kwa kuwawekea wenzao pingamizi ambazo baadaye zinabainika kuwa za uongo, imeelezwa.

Pamoja na kutakiwa kuzisoma kwa kina sheria hizo, wameelezwa kuanza kuwachukulia hatua baadhi ya wanasiasa, kwa kuwafungia kupiga au kupigiwa kura kwa miaka mitano, kwa mujibu wa sheria endapo watabainika kutoa ushahidi na pingamizi za uongo mahakamani.

Jaji Mkuu Augustino Ramadhani, alisema hayo jana, Dar es Salaam wakati akifungua warsha ya siku tatu kwa mahakimu wafawidhi wa mikoa yote nchini iliyoandaliwa na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kuhusu Uchaguzi Mkuu.

Katika hotuba yake, alikiri kuwa majaji na mahakimu wengi hawazijui sheria za uchaguzi na kwamba hali hiyo imesababisha watu kuichezea Mahakama, jambo linalopaswa kukomeshwa haraka.

“Kwa mfano wa Jimbo la Mwibara, waliwahi kukaa bila Mbunge kwa miaka minne, kila aliyeshinda aliwekewa pingamizi, sasa watu hawa wanakuja wanaapa mahakamani kuwa watatoa ushahidi wa kweli tena kweli tupu, lakini kumbe ni uongo, hili linabainika baadaye wakati wananchi wameshateseka,” alisema Jaji Mkuu na kuongeza:

“Sheria imeipa mamlaka Mahakama kuwafungia watu wa namna hii kupiga au kupigiwa kura kwa miaka mitano, na hili linapaswa kutekelezwa, maana watu wanachezea Mahakama, watu wanaapa kwa Biblia na Kurani, lakini kumbe wanasema uongo.”

Alisema mtu anakuja mahakamani kutoa ushahidi, kwamba alipewa rushwa na mgombea fulani na kuapa, lakini anasahau kwamba naye ni mtuhumiwa kwa mujibu wa sheria, ingawa ni shahidi.

Alisisitiza kuwa, mahakimu wanapaswa kuzisoma sheria ili kutatua matatizo ya namna hiyo ambayo ni mengi mahakamani.

Kwa upande wao, washiriki walikiri pia kuwa hawazijui sheria za uchaguzi kwa kuwa hawafundishwi vyuoni na kuongeza:

“Binafsi naona ni wakati muafaka UNDP wanatupiga msasa, ingawa wamechelewa, lakini si mbaya kwa kuwa tulio wengi hatuzijui kabisa hizi sheria za uchaguzi,” alisema Richard Kabate, Hakimu Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro.

Kabate alishauri semina hiyo isiishie kwa mahakimu wa ngazi za mkoa, bali iende mpaka wilayani, kwa kuwa sheria inatoa mamlaka kwao pia kusikiliza kesi zitokanazo na uchaguzi wa kisiasa sambamba na kuwataka mahakimu waliopata mafunzo, kuyaendeleza kwa wenzao, ili matunda ya semina hiyo yaonekane.

Awali Mkurugenzi wa UNDP nchini, Philippe Poinsot, alisema ni muhimu mahakimu kuelewa vyema namna ya kushughulikia mashauri yatokanayo na uchaguzi, kulingana na sheria zake, kwani itasaidia kuepuka vurugu na kuwezesha kushughulika na masuala ya maendeleo na mapambano dhidi ya umasikini nchini.

Wednesday, September 22, 2010

PARIS HILTON ADUWAA KUPIGWA STOP JAPAN….!!!!


Kutokana na habari zilizo tolewa na kituo maarufu cha Cnn ni kwamba mwanadada huyo marufu na mtoto wa mmiliki wa mahotel ya Hilton amepigwa STOP kuingia nchini humo. Na sababu kubwa ni kutokana na tuhuma zinazomkabili za kukutwa na madawa ya kulevya huko nchini Paris na hata huko nchini kwake Marekani katika jiji la Las vegas.

“Alikuwa anataka kuingia Japani kwa ajili ya maswala yake ya kibiashara sana sana katika upande wa kuifanyia masoko lebo yake inayotumika katika bidhaa zake kama manukato” alisema msemaji wake. Mwanadada huyu alikamatwa kwa kosa la umulikaji wa madawa ya kulevya na kumtishia polisi ambapo kosa la kumiliki madawa lilifutwa na kupewa adhabu ya kulipa faini dola 2,000 na kufanya shughuli za kijamii kwa masaa 200.

Lionel Messi kutocheza kwa wiki mbili!!


Lionel Messi ameumia kiwiko cha mguu wakati Barcelona ilipoilaza Atletico Madrid mabao 2-1 katika mchezo wa ligi ya Hispania maarufu La Liga.

Mshambuliaji huyo anayechezea pia timu ya taifa ya Argentina, alitolewa nje kwa machela kipindi cha pili baada ya kuchezewa rafu na mlinzi wa Atletico Tomas Ujfalusi na kuna uwezekano hatacheza soka kwa wiki mbili zijazo.
Taarifa rasmi ya Barca kupitia mtandao wa klabu hiyo imethibitisha Messia ameumia kiwiko cha mguu wa kuume, lakini hakuna mfupa uliovunjika.
Mchazaji huyo bora wa dunia wa mwaka anatazamiwa kufanyiwa vipimo Jumatatu kubainisha ukubwa wa kuumia kwake.

Licha ya Ujfalusi kuoneshwa kadi ya pili ya manjano kwa rafu hiyo, kocha wa Barcelona Pep Guardiola alimshutumu mwamuzi David Fernandez Borbalan.
Guardiola ameongeza kusema kimsingi, Messi hakuvunjika suala ambalo lilikuwa likiwapa mashaka. Baada ya vipimo watafahamu ukubwa wa tatizo.
Picha za televisheni zinajieleza. Si Cristiano Ronaldo pekee anayehitaji kulindwa, waamuzi wanahitajika kuwalinda wacheza wote.

Messi anatazamiwa kukosa michezo ya ligi dhidi ya Sporting Gijon, Real Mallorca na Athletic Bilbao pamoja na pambano la ubingwa wa Ulaya dhidi ya Rubin Kazan tarehe 29 mwezi wa Septemba.

Mshambuliaji huyo aliipatia bao la kuongoza katika dakika ya 13 katika uwanja wa Vicente Calderon, lakini Raul Garcia akasawazisha dakika 11 baadaye.
Mabingwa hao wa Hispania walikosa nafasi nyingi za kufunga kabla Gerard Pique kufanikiwa kuipatia bao la pili na kuzoa pointi zote tatu kwa shuti kali la karibu

Tuhuma za wizi wa kura zagubika uchaguzi wa bunge nchini Afghanistan


Uchaguzi wa bunge la Afghanistan ulimalizika jana jioni ukigubikwa na machafuko na tuhuma za wizi wa kura.

Kamisheni Huru ya Uchaguzi ya Afghanistan imetangaza kuwa asilimia 40 ya watu waliotimiza masharti wameshiriki katika uchaguzi huo. Taarifa ya kamisheni hiyo imesema kuwa uchaguzi wa bunge umefanyika katika asilimia 92 ya ya vituo vya kupigia kura. Vilevile serikali ya Afghanistan imepongeza uchaguzi huo ikisema kwamba ulikua huru na wa haki. Hata hivyo mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Afghanistan Staffan di Mistura ametangaza kuwa takwimu za idadi ya watu walioshiriki kwenye uchaguzi huo zinatia wasiwasi kutokana na hali mbaya ya usalama. Vilevile kumekuwepo kesi za wizi na udanganyifu katika vituo vingi na maeneo mbalimbali ya kupuigia kura.

Kundi la Taliban liliwataka wananchi kususia uchaguzi wa bunge wa Afghanistan na kutishia kushambulia vituo vya kupigia kura. Watu wasiopungua 10 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika ghasia zilizoandamana na uchaguzi huo.

Maelfu waandamana London kupinga safari ya Papa Benedict nchini Uingereza


Maelfu ya watu waliandamana jana mjini London kupinga safari ya Papa Benedict XVI nchini Uingereza wakimtaka Kiongozi wa Kanisa Katoliki kufichua majina ya makasisi waliohusika katika kashfa ya kuwanajisi watoto wadogo, kuweka wazi mafaili yao na kuwafikisha mahakamani.

Watu wasiopungua elfu 12 waliandamana jana katika mitaa ya London wakibeba mapango yanayolaani uhalifu wa makakasisi wa Kikatoliki na kutoa wito wa kulindwa watoto na si kuwakingia kifua makasisi.
Safari ya Papa Benedict XVI nchini Uingereza imeandamana na mashambulizi makali ya vyombo vya habari dhidi ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki na fedheha ya makasisi ya kuwanajisi watoto wadogo.

Maelfu ya askari usalama wa Uingereza wanashiriki katika operesheni ya kulinda amani ya Papa Benedict XVI ambayo imegharimu pauni milioni moja na nusu. Inakadiriwa kuwa gharama za safari ya Papa nchini Uingereza zitafikia pauni milioni 20 zikiwemo pauni milioni 12 za walipa kodi.

Sunday, September 19, 2010

WANANCHI WANGU KUNYWENI POMBE NA MVUTE SIGARA KWA WINGI, ASEMA WAZIRI WA URUSI


Nchi ya urusi ni miongoni mwanchi zinazoongoza duniani kwa unywaji pombe. Na sasa Waziri wa fedha wa nchi hiyo ametoa kali baada ya kuwataka wananchi kunywa pombe kwa wingi na kuvuta sigara zaidi ili kusaidia kukuza uchumi wa nchi hiyo.

Ingawa mara nyingi wanasiasa huwataka wananchi kuzingatia afya bora, bwana Kurdin amewataka wananchi wake kupiga tungi na kuvuta sigara zaidi ili mapato ya taifa yaongezeke. “Ukivuta pakiti moja ya sigara, inamaanisha unasaidia kutatua matatizo ya kijamii” amesema waziri Kurdin. “Watu lazima waelewe, wale wanaokunywa na wavutaji, wanasaidia sana kujenga nchi”.

Hii ni kali, labda wakati anaongea haya, na yeye alikuwa ameshapombeka kidogo.

MATRAFKI WAPENDAO RUSHWA WAPIGWA CHENGA KWA MTANDAO


Hii imetokea huko nchini south Africa ambapo jeshi la polisi limetishia kumkamata na kumshitaki mtu anaetumia mitandao ya twitter na facebook kuwaonya waendesha magari au kuwapa tarifa zihusianazo na mahali walipo matrafiki. Baadhi ya watu huzikwepa barabara hizo na kuwaacha wapenda rushwa hao wakiwa wanakodoa macho kwa kukosa kitu kidogo kutoka kwa madereva.

Jamaa huyo kupitia mitandao hiyo anajiita “PIGSPOTTER”na anafanya hivyo kwa lengo la kupigana na rushwa iliyokithiri katika barabara za nchi hiyo. Akiwa anatumia simu aina ya blackberry anawataarifu waendesha magari na watumiaji wa mitandao hiyo maeneo mbalimbali yanayokuwa na mapolisi.

Katika kukubalika kwa kazi anayoifanya wananchi wametokea kumtetea, na yeye anasema anawaheshimu sana mapolice wanaofanya kazi zao vizuri lakini kwa wale walarushwa wasahau kuipata heshima yake.

KIM KARDASHIAN NA LADY GAGA WAIJIA JUU KAMPUNI YA KUTENGENEZA WADOLI



Ni baada ya kampuni mmoja kutengeneza madoli ya kufanyia mapenzi inayofanana na masupastaa hao.
Kim kardashiani pichani ameitaka kampuni hiyo kusimamisha uzalishaji huo.

Mwanasheria wa mwanadada huyo ajulikanae kwa jina la Shawn Chapman Holley amewandikia barua kampuni ya Pipedream Products, Inc inayoonyesha orodha ya masupastaa ambao wametengenezewa midoli ya aina hiyo na kwamba kampuni hiyo inachokidai kuwa haikufanya makusudi ni uwongo.

Wakati huo huo mwanamziki alie nyanyasa katika tuzo za MTV Video musia awards Lady Gaga amesema ataishitaki kampuni hiyo kwa kuvunja hatimiliki na kuwa sisitiza waondoe picha za madoli walioyaweka katika mtandao wa intanenti.

MLIPUKO WA MAPIPA WAUA 70 SRILANKA



Habari kutoka Sri Lanka zinasema zaidi ya watu 70 wamepoteza maisha yao katika mlipuko wa mapipa matatu yaliyokuwa yamesheheni madini ya dynamite karibu na mji wa Batticaloa, mashariki mwa nchi hiyo. Msemaji wa jeshi la nchi hiyo Meja Jenerali Ubaya Medawela amesema kuwa, mapipa hayo yaliyokuwa na madini hayo hatari, yameripuka ghafla katika kituo cha polisi cha Karadiyanaru, kilomita 260 mashariki mwa Colombo na kusababisha maafa hayo.

Ameongeza kuwa, raia wa nchi hiyo na wajenzi 2 raia wa Uchina ni miongoni mwa walioaga dunia katika ajali hiyo.
Madini hayo yaliyokuwa yamehifadhiwa katika kituo cha polisi kwa sababu za usalama, yalikusudiwa kutumika katika ujenzi wa barabara, mradi ambao ulikuwa umepewa shirika moja la Kichina.

KIBAKA AKIONA CHA MOTO, AIVISHWA AKIWA ANAJIONA!


KIBAKA mmoja ambaye hajafahamika jina lake wala makazi ameuawa kikatili na wananchi wenye hasira kali na kisha kuchomwa moto baada ya kufanya jaribio la kuvunja duka na kuiba bidhaa mbalimbali. Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia juzi majira ya saa 10 alfajiri katika eneo la Mwenge Manispaa ya singida ambapo kibaka huyo alikuwa na wenzake watano. Kwa mujibu wa watu walioshuuhudia tukio hilo walisema kuwa vibaka hao wakiwa watano waliingia katika duka moja la Daniel Miyanji na kuanza kuvunja mageti ya duka hilo kisha kutoa bidhaa mbalimbali zikiwemo bia.

Mdogo wa mmiliki wa duka hilo Daniel Miyanji alisema akiwa amelala usiku huo alisikia kelelele za mbwa wa jirani wakibweka mfululizo. "Baada ya kusikia kelele za mbwa wa jirani muda mrefu niliamka na kuchungulia dirishani na kuona watu wakitoa vitu dukani kwetu, ndipo nilimwamsha kaka yangu na watu wengine juu ya tukio hilo." alisema.

Miyanji alisema kuwa hapo ndipo waliungana na kuanza kuwakurupua vibaka hao ambapo katika kurupushani hizo walifanikiwa kumkamata kibaka aliyekuwa ndani ya duka akitoa mali kwa wenzake na kuanza kushambuliana. Alisema kuwa kibaka huyo alikuwa akiwatisha kwa kisu lakini kutokana na umoja wa wananchi waliofika kutoa msaada baada ya kupiga makelele walimzidi nguvu na hatimae kuanza kumshambulia.

WATANO MBARONI KWA UGAIDI DHIDI YA PAPA BENEDICT


Polisi mjini London wanawashikilia watu watano kuhusiana na taarifa za uwezekano wa kuwepo tishio la kigaidi dhidi ya Papa Benedict.
Watu hao walikamatwa mjini London mwishoni mwa wiki baada ya maafisa wa kupambana na ugaidi kupokea taarifa za kijasusi kuhusu kuwepo kwa tishio hilo.
Watu hao wamepelekwa katika kituo kikuu cha polisi mjini London.
Maafisa wanaendelea na uchunguzi wao katika maeneo ambayo yanashukiwa kufanyika uvamizi unaohusiana na tishio hilo.

Katika taarifa iliyotolewa na Kikosi cha Scotland Yard, Polisi wanasema watano hao wamekamatwa katika msako uliofanywa na maafisa katika kamandi ya kupambana na ugaidi.
Wanashikiliwa kwa tuhuma za kupanga, kuandaa au kushawishi vitendo vya ugaidi chini ya sheria ya ugaidi ya mwaka 2000.
Umri wao ni miaka 26, 27, 36, 40 na 50. Walikamatwa katika maeneo ya biashara ambako msako ulikuwa ukifanyika.
Maeneo ya makazi kaskazini na mashariki mwa London pia yanafanyiwa msako.

PRESIDENT JAKAYA AMPIGA TAFU LOWASSA MONDULI


Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Jakaya Kikwete, akimnadi mgombea ubunge jimbo la Monduli mkoani Arusha, Edward Lowasa, kwa wapiga kura wa jimbo hilo wakati wa mkutano wa kampeni jana jioni.


Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dr.Jakaya Kikwete, akihutubia wananchi wa jimbo la Monduli mkoani Arusha jana jioni.

Friday, September 17, 2010

mtangazaji wa radio free afrika avamiwa,ajeruhiwa vibaya.!


MTANGAZAJI WA RADIO FREE AFRIKA AMBAYE VILEVILE YU PRODUCER WA KUREKODI MUZIKI WA KIZAZI KIPYA NDANI YA TETEMESHA PRODUCTION SANDU GEORGE MPANDA MAARUFU KWA JINA LA KID BWAY AMEVEMIWA NA KUPIGWA NA KITU KIZITO KICHWANI.

TAARIFA ZINASEMA KUWA KID BWAY AKIWA NYUMBANI KWAKE LUMALA JIJINI MWANZA, JAMAA ALIYEMVANIA ALIFIKA NYUMBANI HAPO MAJIRA YA SAA 2:30 USIKU NA KUJITAMBULISHA KAMA MSANII AKIHITAJI KUFANYA RECORDING, BAADA YA MAZUNGUMZO NA KUJITAMBULISHA ALIKARIBISHWA NDANI HADI CHUMBA CHA KUREKODIA STUDIO.

NYUMBANI KWA MTANGAZAJI HUYO ANAISHI NA JAMAA ZAKE WAWILI AMBAO WAKATI KID AKIMKARIBISHA MTENDA UHALIFU HUO NYUMBANI HAPO JAMAA HAO WALIMWONA KIJANA HUYO KISHA KILA MMOJA AKAINGIA CHUMBANI KWAKE. DAKIKA KADHAA WAKASIKIA KWA KIPINDI KIREFU SPIKA ZA STUDIO ZIKIKOROMA ISIVYO KAWAIDA NA KUANZA KUDADISI HUKU WAKIMWITA KID BWAY KUWA INAKUWAJE! WAKAITA NA KUITA NDIPO WALIPO AMUA KUINGIA STUDIO NA KUMKUTA SAKAFUNI KAANGUKA DABU ZIKIMTOKA MASIKIONI, PUANI NA KWENYE MAJERAHA SEHEMU ZA KICHWA.

KWA HIVI SASA KID YUPO HOSPITALI YA RUFAA BUGANDO AKIWA HOI HAJITAMBUI YAANI KAPOTEZA FAHAMU, ALITUNDIKIWA DRIPU YA MAJI IKIWA NI HUDUMA YA KWANZA AMBAYO AMEPATIWA JANA MARA BAADA YA KUFIKA HOSPITALINI HAPO AKISUBIRI KIPIMO CHA T SCAN KUONA KWA UNDANI ZAIDI SEHEMU ALIZODHURIKA. HAKUNA TAARIFA YOYOTE YA UPOTEVU WA MALI HALI INAYOPELEKEA WADADISI WA MAMBO KUDHANI KUWA YAWEZEKANA KULIKUWA NA VITA YA KICHINI CHINI AKA BIFU(AMBAYO HAIJAFAHAMIKA).

UCHUNGUZI KWA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI UNAENDELEA KUJUA NINI SABABU ZA UVAMIZI HUO.

TAARIFA ZAIDI TUTAENDELEA KUKUJULISHA.
TWAMWOMBA MWENYEZI MUNGU AKUPE NGUVU BROTHER UPATE KUPONA.


Habari hii ni kwa hisani ya mdau G Sengo.

NIACHENI JAMANI NIMECHOKA


Jamaa huyu amenaswa na kamera yetu maeneo ya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam akiuchapa usingizi mchana wa leo kama ambavyo anaonekana baada ya mihangaiko ya hapa na pale ya kutafuta maisha.

Nakaaya Sumari aikacha CHADEMA, ajiunga CCM!


Mwanamuziki wa kizazi kipya nchini ambaye alikuwa Mwanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) mkoani Arusha, Nakaaya Sumari, jioni hii ametangaza kukihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Nakaaya katangaza hayo jioni hii mbele ya mgombea urais wa CCM,Dr. Jakaya Kikwete katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha wakati wa mkutano wa kampeni za Wilaya ya Arumeru

Wednesday, September 15, 2010

LULU ALEWA CHAKARI SIKU YA IDD MOSI!!




Awali wawili hao walikutwa na kamera yetu ndani ya Ukumbi wa Sun Sirro uliopo Shekilango Ubungo jijini Dar ambapo kulikuwa na uzinduzi wa kundi la Tip Top Connection na baadaye kuibukia katika Klabu Billicanas.

Akiwa ‘Bills’ na ‘shosti’ wake walizidi kugida bia na kadri muda ulivyozidi kusogea mbele ndani ya ukumbi huo, ndivyo Lulu alivyokuwa akionekana kulemewa kimtindo.





Kati ya watu waliokuwa karibu yao ni ‘Pedeshee’ mmoja mwenye asili ya Kihindi ambaye alijipendekeza kwa Lulu kwa kulipia vinywani na vilaji akiwa na lengo la kuondoka na msanii huyo kwenda naye anakokujua yeye.

Hata hivyo, ilifika mahali Lulu alzidiwa na pombe hizo na kuonekana kama vile alikuwa akitaka ‘kuangusha gari’


Ilifikia hatua Lulu aliamua kutafuta sehemu ya kuegemea kutokanana kuzidiwa na pombe na kuinamisha kichwa kulala huku ‘Kanjibai’ huyo akiwa anemmezea mate pembeni yake.

Baadaye msanii huyo aliyekuwa mguu kwa mguu na shostito wake walishtukia mtego wa Pedeshee huyo wa Kihindi na kumtoka kiaina wakimwmabia wanatoka kidogo



Mdosi baada ya kubaini kwamba ameachwa ‘njia panda’ alionekana akizagaazagaa huku na kule kumsaka msanii huyo na shoga yake lakini bila ya mafanikio kwani kwa wakati huo ilishatimu saa kumi na moja kasoro robo alfaajiri ambapo Lulu na shoga yake walichomoka na kuelekea pande za Sinza Makaburini.


‘Shosti’ wake Lulu.

Kamera yetu ilipowakimbiza pande hizo iliwakuta wamepiga kambi kwenye hoteli moja (jina tunalo) na baadaye kuelekea makwao huku wakiwa katika gari aina ya Hiace nyekundu iliyokuwa na wanaume wanne kama mabaunsa wao.

Sunday, September 12, 2010

COCO BEACH YAFURIKA,UANGALIZI WA WATOTO HAUKO MAKINI


Ni katika moja na mbili watu walikuwa wamepozi kwenye mapango wanabadilishana mawazo!hii ni siku ya idd mosi cocobeach

HATA KAMA NI NIA HAITANGAZWI HIVI!!!:::::::


...raha ikizidi jamani ni balaa!...

Wednesday, September 8, 2010

John Mnyika anaomba umchangie amudu gharama

CHADEMA yaazimia kuishitaki CCM kwa Wapiga Kura


L-R: Mabere Marando | Prof. Mwesiga Baregu | John Mnyika
Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Kampeni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Prof. Mwesiga Baregu akiwa na viongozi wengine wa chama hicho, leo katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam amezungumzia maamuzi ya Msajili wa Vyama vya siasa nchini kutupilia mbali malalamiko ya chama hicho dhidi ya mgombea wa Uraisi kupitia CCM, Jakaya Kikwete.

Amesema CHADEMA imeweka wazi kuwa haitaweza kwenda mahakamani kutaka mgombea Uraise kupitia CCM, Jakaya Kikwete, aenguliwe kushiriki uchaguzi na badala yake watawashawishi wananchi wasimpigie kura mgombea huyo wa CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Uamuzi CHADEMA unakuja baada ya wakili wa chama hicho ambaye pia ni mjumbe wa timu ya Taifa ya kuratibu kampeni za uchaguzi, Mabere Marando, kutoa ushauri wa aina mbili ambao ni, kwenda Mahakama kuu kuomba marejeo ya maamuzi ya Tendwa ili mahakama hiyo itoe maamuzi ya haraka ya kumuondoka Rais Kikwete kugombea Uraisi au; Kushitaki kwa kutumia sheria ya gharanma za uchaguzi.


credit source: http://www.wavuti.com/habari.html#ixzz0yvXkVguQ

Nimemaliza Shule!


BAADHI ya watahiniwa katika shule ya Msingi, Miburani, Temeke, Dar es Salaam wakishangilia baada ya mtihani wa mwisho wa kuhitimu Elimu ya Msingi. (photo: Bashir Nkoromo).
Vijana hawa wananikumbusha siku tuliyokuwa tukiisubiri kwa hamu kubwa sana, 'kumaliza shule' tukiamini ati baada ya kuondokana na adha ya kudamka alfajiri, kushikana mashati na 'konda', kuwahi 'namba' na 'mstarini'... yaani ndoto za kila aina alimradi kujiaminisha usumbufu utakuwa umekwisha kabisa.

Tulijiona sisi ndiyo 'top' hakuna mwingine duniani kama sisi. Hisia za 'kumaliza shule' na kubaki nyumbani wakati wengine wanaamka asubuhi wakiwa na heka heka za ama kwenda shuleni au kazini, zilitutawala.

Siku hizi, tofauti na zamani nilipomwona 'madha mnoko', huwa najivuna sana kuwa na Mama asiye na longolongo wala 'kukopesha maneno' kwani, aliponisikia nikijitapa eti 'nimemaliza shule' siku moja aliniambia,

"...wewe, umemaliza shule ipi? Subi, hujamaliza shule. Umehitimu Elimu ya Msingi tu. Umeimalizaje shule wakati hujafika hata Sekondari? Umesahau methali mlizofundishwa, Elimu ni bahari; Elimu haina mwisho? au ulidhani ukishakariri na kuandika kwenye daftari ukafunga na ulichofundishwa kimefungwa kwenye mkoba? Yaani mwalimu akishafuta ubao na kwenye akili yako vinafutika? (kichwani mwangu nawaza, 'kwani si ndiyo kazi ya shule? unaandika, mnakusanya madaftari, mwalimu anatia 'pata' kama hesabu umekosea fanya masahihisho tu, basi').

Umevuka madarasa ya shule ya awali, sababu ya kuitwa 'msingi' ni kwa kuwa umeweka msingi wa elimu na maisha yako. Ni sawa na kujenga nyumba. Ili iweze kusimama imara, lazima msingi uwepo, tena uwe ni msingi ulio imara. Msingi ndiyo kigezo cha uimara wa nyumba. Umeweka msingi, bado kuta, madirisha, paa, na fenicha na vifaa vingine vya ndani. Lakini la muhimu ni msingi. Ikiwa uliweka msingi imara, nyumba yako itakuwa imara, utaweza kujenga nyumba kuuuubwa au hata orofa, inategemea na uimara wa msingi wake."

Ni baada ya kwenda kwa Bibi na kuwatembelea ndugu, ninarejelewa kauli ya Mama, 'hujamaliza shule' nhe he, ndipo nilipotia akilini, kumbe tulichokuwa tukifurahia 'standadi seven kumaliza shule' ilikuwa ni furaha ya muda tu, tena ya kitoto, bado ilikuwepo kazi kubwa mbele yetu; Kuna kusaidia kazi za nyumbani sasa zaidi ya wengine na; Kuna kuchukua fomu za shule za "private" tena kujaza zaidi ya moja, na kwa ambaye matokeo ya maendeleo yake shuleni kila mhula hayakuwa mazuri, hali kwake ilikuwa ni mbaya, yaani atazijaza fomu za 'private school' hata tano ili walao abahatishe moja ikiwa atakataliwa kwingineko. Nakumbuka nilizijaza mbili, Majengo Secondary na Uru Seminary. Kisha kuna kufanya tena mtihani wa kuomba kujiunga na shule hizo na, ni lazima ufaulu, la sivyo uaibike kwa kuzurura mtaani na kufanya kazi nyumbani wakati wenzio wanaongozana kwenda na kutoka shuleni! Shabash! Hakuna kumaliza shule!

Naam, huo ndiyo wakati nilipoanza kufahamu kuwa ninayahama maisha ya utoto na kuingia ujanani.

Hongereni vijana mliohitimu elimu ya msingi, shule bado hamjaimaliza. Elimu haina mwisho

Msuba. Ganja. Bangi. Marijuana. Jani. Hashish. Charas.

Cpl Ryan Belgrave with the Canadian Army's 1st Battalion, The Royal Canadian Regiment Battle Group, walks through a field of marijuana plants during a patrol near the village of Salavat, in the Panjway district west of Kandahar on August 4, 2010. (REUTERS/Bob Strong)
Picha, hii inawakilisha sehemu ndogo sana tu ya mashamba yote ya bangi yaliyomo nchini Afghanistan.

Ukitaka kusoma matumizi ya bangi kwa ajili ya matibabu,

Hayo ni majina kadhaa yaliyopewa mmea wa 'bangi' ambao unahesabiwa kuwa mojawapo ya madawa ya kulevya ingawaje wengine husema kuwa majani yake ni mboga ya kawaida tu kwa ugali isiyo na madhara.

Hadi kufikia mwezi Machi 2010, takwimu zilizoripotiwa na Umoja wa Mataifa zinasema kuwa Afghanistan ndiyo nchi inayoongoza duniani kwa kilimo na uzalishaji wa mmea wa bangi ambapo nusu ya majibo yote 34 ya nchini humo hujishughulisha na kilimo cha mmea huo ambapo inakadiriwa kuwa hekta moja huzalisha kilo 145 ya bangi tofauti na kilo 40 zinazozalishwa kwa ukubwa wa eneo ilo hilo huko Morocco. Inakadiriwa pia kuwa kiasi cha dola za Kimarekani $3,900 hupatikana katika mauzo ya hekta moja ya bangi.


Mrema azungumzia kazi ya kubeba zege


Mgombea ubunge kupitia tiketi ya Tanzania Labour Party (TLP), Agustine Lyatonga Mrema.
MGOMBEA ubunge kupitia tiketi ya Tanzania Labour Party (TLP), Agustine Lyatonga Mrema katika jimbo la Vunjo Moshi Vijijini, amesema kwamba kazi ya ubunge siyo sawa na kazi ya kubeba zege ambayo itawahitaji vijana na siyo watu wazima kama yeye.

Mgombea huyo aliyasema hayo katika kipindi cha Mchakato Jimboni kinachorushwa na Runinga ya TBC1 kilichofanyika Chuo cha Ualimu Marangu hivi karibuni ambapo Mrema aliulizwa swali na mwananchi mmoja aliyetaka kujua kutokana na umri wake mkubwa na madai kwamba ni mgonjwa, je ataweza mikikimikiki ya kuwahudimia wananchi hao vyema kama wakimpa nafasi ya kuwa mbunge.

“Bungeni hatuendi kubeba zege,” alianza kujibu Mrema na kuwafanya watu waliohudhuria mdahalo huo kulipuka kwa vicheko na kuendelea kutamba kwa kusema kwamba yeye anaijua kazi hiyo vizuri sana tofauti na wagombea wengine kwa kuwa aliwahi kuwa Mbunge wa jimbo hilo kwa kipindi cha miaka 10 hivyo anapaswa kupewa kura za wananchi wa jimbo hilo la Vunjo.

“Watu wanasema sijui Mrema anaumwa, mtu huwezi kukwepa kuumwa hata Dk. Slaa (Dkt. Willibrod Slaa mgombea urais wa Chadema) aliumwa pale alipoanguka bafuni na kuumia mkono, sijui nini si mnaniona au kama mnaona mimi ni mgonjwa muulizeni mke wangu kama kweli mimi ni mzima au mgonjwa…” alisema Mrema na kumfanya mwendesha kipindi hicho Shaaban Kissu kumkatisha kwa kumwambia kuwa inatosha.

Mbali na Mrema wagombea wengine waliojitokeza katika mdahalo huo ni pamoja na John Mrema wa Chadema na Crispine Robert Meela wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao nao kama ilivyokuwa kwa Mrema walipata fursa ya kutangaza ilani za vyama vyao.

BREKING NYUZZZZZ:DR. SLAA AFUNGULIWA MASHTAKA MAHAKAMA KUU JANA


MGOMBEA urais kwa tiketi ya CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa (pichani), amefunguliwa kesi katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaami, akidaiwa fidia y ash. bilioni moja kwa madai ya kunyang’anya mke wa mtu.

Kesi hiyo namba 122 ya mwaka 2010, ilifunguliwa leo mahakamani hapo na Aminiel Mahimbo kwa kupitia ofisi ya mawakili ya Amicus.

Mahimbo anadai kuwa, Dk. Slaa kamnyang’anya mkewe wa ndoa Josephine Mushumbusi.

Kwa kupitia nakala ya hati ya madai, Mahimbo anadai fidia ya sh. milioni 200 kutokana na hasara alizozipata baada ya mdaiwa huyo, kumtangaza mkewe wa ndoa Josephine kuwa mchumba wake na sh. milioni 800 ikiwa ni hasara ya jumla aliyopata.

Mlalamikaji huyo, anadai Septemba 7, 2002 alifunga ndoa na mwanamke huyo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ushirika wa Kijitonyama na kuishi maeneo mbalimbali ikiwemo Kimara, Baruti, Dar es Salaam.

Pia anadai katika maisha yao ya ndoa wamebahatika kuwa na watoto wawili ambao ni Upendo aliyezaliwa Mei Mosi, 2003 na Precious aliyezaliwa Machi 14, 2007.

Mahimbo alidai, ndoa kati yake na Josephine haijavunjwa na chombo chochote na kwamba, bado ni mke wake halali.

Kwa mujibu wa hati hiyo, Mahimbo alidai hivi karibuni, mkewe alikuwa na safari za mara kwa mara na aliamini ni za kikazi. Josephine ni mfanyabiashara ambaye anaendesha kampuni iitwayo Green World Clinic.

Alidai katika tarehe na mahali tofauti, Dk. Slaa alimtambulisha mwanamke huyo kuwa ni mkewe, suala ambalo si kweli.

Mlalamikaji huyo alidai, uhusiano uliopo kati ya watu hao wawili umemfanya adhalilike na kunyanyasika katika jamii na anaiomba mahakama kumzuia Dk. Slaa kuendelea kujihusisha kimahusiano na mkewe.

Anaiomba mahakama kumwamuru Dk. Slaa kumlipa bilioni moja na kulipa gharama za kuendeshea kesi.

Mahimbo amedai ameambatanisha na cheti cha ndoa na Josephine, picha za harusi, vyeti vya kuzaliwa vya watoto na nakala za vipande vya magazeti zilizopigwa wakati Dk. Slaa akimtambulisha mwanamke huyo kuwa ni mkewe.

Tuesday, September 7, 2010

Upendo Nkone Kufunga Ndoa Tarehe 17 October 2010


Muimbaji wa Injili Upendo Nkone atategemea Kufunga ndoa tarehe 17 October 2010 na Mchungaji John Mbeyela ambaye pia ni mjane mwenye watoto watatu, ndoa hiyo itafungwa katika kanisa la Naioth kwa Mchungaji Mwasota.
Akiongea na Strictly Gospel Upendo Anasema “Ninafurahi sana na ninaomba Mungu akamfute machozi kila mjane, haijalishi umekaa miaka mingapi. Mungu yupo atakukumbuka”
Bi. Nkone ambaye ameishi maisha ya ujane kwa miaka 9, ana jumla ya album tatu ambazo ni Mungu Baba, Hapa Nilipo na Zipo faida.
Tunamtakia kila la heri katika maandalizi yote mpaka harusi

JAMANI DADA ZETU MNAAIBISHA MAMA ZETU WAPENDWA!!


Hii picha nimetumiwa na mdau wa blogu hii ya umbea.com akiwashutumu kina dada zetu juu ya tabia zao za kwenda kwenye starehe pasipo kuvaa hata nguo za ndani kiukweli baada ya kulewa matokeo yake ni kama haya kujiachia mbele za watu na watu kula kideo mfano mzuri mcheki huyo jamaa picha anavyokodoa macho.je wadau nani wakulaumiwa hapa!!

MSANII WA KIKE WA KIPEKEE NCHINI KWA SASA ALIYEFUNIKA KWENYE PRETTY GIRL

Huyu ndiye Irene a.k.a ndikumana anayetesa katika filamu mbalimbali za RJ company inayomilikiwa na ray na johari hivi karibuni watatoa filamu yao inayokwenda kwa jina la pretty girl hivyo basi nawaonjesheni wadau wangu japo kidogo tu baadhi ya picha au madoido yaliyo kwenye movie hiyo wadau wangu yani hata mie natamani kuiona hebu rj company fanyeni tu haraka jamani muitoe hiyo filamu basi!




Akiwa mbele ya JEEP




Unaniona?






Ni kweli PRETTY?


Ndani ya bustani
Msubiri umuone alivyoharibu mbaya katika PRETTY GIRL