Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Thursday, April 22, 2010

AMWIK WATOA MAFUNZO YA HAKI ZA WANAWAKE NA WAJIBU WAO KWA SERIKALI NCHINI KENYA!!


Kina mama wa kabila la Kiturukana wakiwa na nyuso za furaha mara baada ya kupata mafunzo ya haki za wanawake. Chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Kenya (AMWIK) kimekuwa kikitoa mafunzo kwa kutumia Community Radio Listening Group kuwaelimisha wanawake hao ili wajue haki zao na wajibu wao kwa serikali.
(Picha na Anna Nkinda -Kenya)

Kundi kubwa la ngamia wakiwa wanakunywa maji katika mto Chicho Hoko ulioko wilayani Isiolo katika Mkoa wa North Estern nchini Kenya. Ngamia hao wanamilikiwa na wafugaji wa kabila la waborana.Hivi karibuni wilaya hiyo ilikumbwa na ukame uliosababisha kufa kwa mifugo mingi wakiwemo ng’ombe, mbuzi na kondoo lakini ngamia ni wanyama wanaostahimili hali ya ukame.

Mdau Lawrence Mureith akiwa amesimama nje ya moja ya nyumba ya kabila la waturukana ambao ni wafugaji wanaopatikana huko wilayini Isiolo mkoani Kenya.

Watoto wa kabila la kiturukana wakiwa na nyuso za furaha wakati wanapigwa picha.

Kina mama wa kabila la Kiturukana kutoka kundi la ANUPIT wakiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa Chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Kenya (AMWIK) mara baada ya mafunzo ya haki za wanawake na wajibu wao kwa serikali yanayotelewa na chama hicho kwa kutumia Community Radio Listening Group.

Wednesday, April 21, 2010

J....MARTINS AFANYA ONYESHO LA NGUVU JANA


Hili ndio jengo lenyewe lililozinduliwa jana kama taswira ya picha inavyoonyesha na stage yake kwa mbele ambapo ndipo j martins atakapo warusha wadau wake na kwa mujibu wa ratiba niliyopata kuwa mambo yalirushwa live na kituo cha ITV NA CHANNEL 5 huku kiingilio kikiwa ni miguu yako tu hahahhahahah.
picha na kachero wa umbea.com

KAMERA YA UMBEA.COM YAMBAMBA KANUMBA AKINUNUA MKANDA


kama mnavyonijua wadau wangu kwa umbea jana mida ya juaa kali nilimbamba msanii huyu akimuunga mkono kijana huyu kwa kununua mkanda kwa ajili ya suruale yake ambalo ni jambo zuri kwa kuwajali vijana hawa wanaouza vitu vidogo vidogo big up sana brother mie nimekuunga mkono

Vyeti Necta kuwekwa picha za mtahiniwa

KUTOKANA na vitendo vya udanganyifu kukithiri kwenye vyeti vya kidato cha nne na cha sita, Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), limeanza kuweka picha katika vyeti vya matokeo ya ngazi hizo za elimu, ili kuwawezesha wadau kumtambua mmiliki halali wa cheti.

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Mwantumu Mahiza, aliliambia Bunge mjini Dodoma kuwa picha hizo huwekwa kwa kompyuta hivyo haziwezi kuondolewa kirahisi na mtu yeyote.

Uwekaji huo wa picha katika vyeti utaanza na vyeti vya watahiniwa waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2008 ambavyo vitachapwa Mei 2010.

Naibu Waziri huyo alisema hati za matokeo ya mitihani ya kidato cha nne 2009 nazo zimetolewa zikiwa na picha.

Alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Konde, Dk Ali Tarab Ali (CUF), aliyehoji kwa nini vyeti vya kidato cha nne na sita visiwekwe picha ya mtahiniwa husika kwa kutumia kompyuta ili kuondoa tatizo la udanganyifu.

Mbunge huyo katika maelezo yake alidai baadhi ya vyeti vya matokeo ya mtihani wa kitaifa ya kidato cha nne na sita kutoka Necta, vinatumiwa na watu wengine wasio watahiniwa kwa ajili ya kutafuta ajira au nafasi za masomo nje.

Katika kujibu swali hilo, Mahiza alikiri kuwa ni kweli kwamba baadhi ya watu wasiokuwa waaminifu wamebainika kutumia vyeti vya matokeo ya mitihani ya kitaifa ya kidato cha nne na sita visivyokuwa vyao, kwa ajili ya kutafuta ajira au nafasi za masomo ya juu, jambo ambalo ni kosa la jinai.

Alitoa mwito kwa wananchi wote kuacha mtindo wa kutumia vyeti visivyokuwa vyao kwani kufanya hivyo kunawanyima wenye vyeti stahili zao na ni kutenda kosa la jinai.

Katila swali lake la nyongeza, Mbunge huyo wa Konde alidai kuwa suala la mtu kutumia cheti ambacho sio chake mara nyingi linafanywa kwa makubaliano na mwenye cheti husika, hivyo alitaka kufahamu pia hatua zinazochukuliwa na Serikali kwa wote walioshiriki kufanya udanganyifu huo.

Lakini kwenye majibu yake, Mahiza alisema kuwa kesi za kuuza cheti ni chache sana na mara nyingi kama Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, wanapata kesi za watu kupotolewa na huwa wanazipeleka Polisi ili zishughulikiwe.

FIXTURE KILI TAIFA CUP - 2010 GROUP 'A' - DODOMA

(a) Dodoma
(b) Kigoma
(c) Singida
(d) U - 20

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Singida V/S U-20 14:00 HRS JAMHURI ST.
2. 5/8/2010 C/D Dodoma V/S Kigoma 16:00 HRS JAMHURI ST.
5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C U-20 V/S Dodoma 14:00 HRS JAMHURI ST.
4. 5/10/2010 D/A Kigoma V/S Singida16:00 HRS JAMHURI ST.

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Singida V/S Dodma 14:00 HRS JAMHURI ST.
6. 12-May-10 D/B Kigoma V/S U-20 16:00 HRS JAMHURI ST.
GROUP 'B' - TANGA
(a) Tanga
(b) Morogoro
(c) Pwani
(d) Temeke

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Tanga V/S Morogoro 14:00 HRS MKWAKWANI
2. 5/8/2010 C/D Pwani V/S Temeke 16:00 HRS MKWAKWANI

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Morogoro V/S Pwani 14:00 HRS MKWAKWANI
4. 5/10/2010 D/A Temeke V/S Tanga 16:00 HRS MKWAKWANI

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Tanga V/S Pwani 14:00 HRS MKWAKWANI
6. 12-May-10 D/B Temeke V/S Morogoro 16:00 HRS MKWAKWANI

GROUP 'C' - MWANZA
(a) Mwanza
(b) Kagera
(c) Shinyanga
(d) Tabora

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Shinyanga V/S Kagera 14:00 HRS C.C.M. KIRUMBA
2. 5/8/2010 C/D Mwanza V/S Tabora 16:00 HRS C.C.M. KIRUMBA

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Kagera vs Mwanza 14:00 HRS C.C.M. KIRUMBA
4. 5/10/2010 D/A Tabora vs Shinyanga 16:00 HRS C.C.M. KIRUMBA

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Shinyanga vs Mwanza 14:00 HRS C.C.M. KIRUMBA
6. 12-May-10 D/B Tabora V/S Kagera 16:00 HRS C.C.M. KIRUMBA

GROUP 'D' - ARUSHA
(a) Arusha
(b) Mara
(c) Manyara
(d) Kilimanjaro

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Mara V/S Kilimanjaro 14:00 HRS SHEKH AMRI ABED
2. 5/8/2010 C/D Manyara V/S Arusha 16:00 HRS SHEKH AMRI ABED

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Kilimanjaro V/S Manyara 14:00 HRS SHEKH AMRI ABED
4. 5/10/2010 D/A Arusha V/S Mara 16:00 HRS SHEKH AMRI ABED

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Mara V/S Manyara 14:00 HRS SHEKH AMRI ABED
6. 12-May-10 D/B Arusha V/S Kilimanjaro 16:00 HRS SHEKH AMRI ABED

GROUP 'E' - IRINGA
(a) Iringa
(b) Mbeya
(c) Rukwa
(d) Kinondoni

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Rukwa V/S Mbeya 14:00 HRS SAMORA ST.
2. 5/8/2010 C/D Iringa V/S Kinondoni 16:00 HRS SAMORA ST.

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Mbeya V/S Iringa 14:00 HRS SAMORA ST.
4. 5/10/2010 D/A Kinondoni V/S Rukwa 16:00 HRS SAMORA ST.

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Rukwa V/S Iringa 14:00 HRS SAMORA ST.
6. 12-May-10 D/B Kinondoni V/S Mbeya 16:00 HRS SAMORA ST.

GROUP 'F' - MTWARA
(a) Mtwara
(b) Lindi
(c) Ruvuma
(d) Ilala

SN - DATE - CODE - TEAMS - TIME - GROUND
1. 5/8/2010 A/B Lindi V/S Ruvuma 14:00 HRS NANGWANA ST.
2. 5/8/2010 C/D Mtwara V/S Ilala 16:00 HRS NANGWANA ST.

5/9/2010 REST DAY

3. 5/10/2010 B/C Ruvuma V/S Mtwara 14:00 HRS NANGWANA ST.
4. 5/10/2010 D/A Ilala V/S Lindi 16:00 HRS NANGWANA ST.

5/11/2010 REST DAY

5. 12-May A/C Lindi VS Mtwara 14:00 HRS NANGWANA ST.
6. 12-May-10 D/B Ilala VS Ruvuma 16:00 HRS NANGWANA ST.

FIXTURE KILI TAIFA CUP - 2010
QUARTER, SEMI FAINAL AND FAINAL
KILIMANJARO TAIFA CUP 2010
FROM 23 MAY, 2010 TO 29 MAY, 2010
UHURU STADIUM - DAR ES SALAAM

SN - DATE - TEAMS - TIME - GROUND
QUARTER FINAL

1. 23 May, 2010 WINNER GROUP 'A' V/s WINNER GROUP 'B' 14:00 HRS UHURU ST - DSM
2. 23 May, 2010 WINNER GROUP 'C' V/s WINNER GROUP 'D' 16:00 HRS UHURU ST - DSM
3. 24 May, 2010 WINNER GROUP 'E' V/s WINNER GROUP 'F' 14:00 HRS UHURU ST - DSM
4. 24 May, 2010 WINNER GROUP 'G' V/s WINNER GROUP 'H' 16:00 HRS UHURU ST - DSM

SEMI FAINAL

5. 25 May, 2010 WINNER GROUP 'A' V/s WINNER GROUP 'B' 16:00 HRS UHURU ST - DSM
6. 26 May, 2010 WINNER GROUP 'C' V/s WINNER GROUP 'D' 16:00 HRS UHURU ST - DSM

27 May, 2010 REST DAY

7. 28 May, 2010 LOOSER No. '5' V/s LOOSER No. '6' 16:00 HRS UHURU ST - DSM
8. 29 May, 2010 WINNER GROUP '5' V/s WINNER GROUP '6' 16:00 HRS UHURU ST - DSM

Tuesday, April 20, 2010

MIAKA HIYO……THOSE WERE THE DAYS! VERY INTERESTING

JIKUMBUSHE NA BARUA ENZI HIZO ZA KISHULE SHULE…LUGHA HAIPANDİ..HALAFU UNAILAZIMISHA IPANDE..BINTI AMEMWANDIKIA BARUA ‘BOIFLENDI’ WAKE..(pichani ndiyo binti)

Dear Sugar
Time and ability plus double capacity has forced my pen to dance automatically on this benedicted sheet of paper. Why! this miraculous thing happened is because papie I love you spontaneously and as I stand horizontal to the wall and perpendicular to the ground I only think of you, since you are a fantastic and fabulous guy.

Papie please Stop haranguing with the feelings in my heart because I love you more than a snake loves the rat. To me each day starts by thinking of you and ends by dreaming of you. Each time I see you, my metabolism suddenly stops and my peristalysis goes in reverse gear. My medula-oblangata also stops functioning.
Crazy crazy crazy you may say but this is true. If only you knew what is going on in my encephalon you would understand. That’s why I need to see you face to face with you, soon. I think I have to pen-off here because I still haven’t finished studying electrolysis and polymerization. Catch you Pa – later. Sleep tight and don’t let those bed bugs ever bite you coz you are too sweet a thing for them.
I have put my beautiful picture in the letter for you.

Yourz Ever,
Sugar nonoza..

BAADA YA YA ’BOIFLENDI’ KUPATA BARUA MAJIBU YAKAWA HIVI…..(pichani ndiyo BF mwenyewe)

Dear Honie
My Love, My Sugar, i was exasperated with pride to have received one from you, the lungs in my body flapped with joy when i have been reading your letter. Anyway by now you have reached the realisations to why i am jotting this small letter to you, yes it is to see if you are keeping with the sands of time.
How is everything on that other side of yours? Well here everything is just half lemon half sugar to make it schweppes. How is your schooling? How are you pulling the wagons of life? I am just pulling the schooling thing like a donkey pulling a cart.

My honie, i am missing you very much right now, my heart is perambulating with every word that i write, if it was not for these oceans that decided to flow between us then i would get on the next bus to come and see you, but until then i know that i will not hesitate to put this blue blood on this paper and write to you. I remember that day lovie, that one sweet day as Maria Curry sanged it, you know that it is my favorites song honie, the one day that we were boarding the combies and you escorted me to my home, walking with you just brought sweet dreams to me for the rest of my life honie.

If words of love could ride a bicycle I would be competing against Diego Maradona. Anyways, i will not stop you from reading the books that give you life and education so I will stop here for today.
Please always writing to me because I am missing you like sugar misses tea. You can see my foto in the letter. My dedications to you are : Maria Curry – One Sweet Day. Boys to Main – And of the Rod.

Keep well my mop of my heart,
Yours in flesh and in blood,
Ruise Sugar Baby.

P.S. Sorry about my english, I did not learn anymore

Stiggo thanks for the email!!!!

HAWA NDIO BAADHI YA WASANII WALIO UWAGA UKAPERA.


Mmoja wa member anayeunda kundi la Wakali Kwanza, Joseph Mapunda a.k.a Qj pichani akiwa na mkewe Bi Elizabeth na kwa sasa wameungana na kuwa kitu kimoja kama Mr and Mrs Joseph Mapunda hii ni juzi tu jamaa kavuta jiko safi.

Huyu ni Matonya siku ya harusi yake hapo akiwa na rafiki yake kipenzi Banana Zoro pamoja na mkewe.. Na kwa kudra zake mwenyezi mungu ndoa hiyo imeshaipa baraka kwa kupatikana mtoto.. Tonya pia ni moja kati ya wasanii wa bongo flava ambao tayari washauwaga ukapera.

Picha juu ni Juma Nature na mkewe Pili siku ya harusi yao .. Sir Juma Nature na mkewe wamebarikiwa kupata mtoto wa kike aliyezaliwa katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke.. Huyu ni Mwingine pia ambaye amesha watoroka wale wengi ambao bado hawajakamilisha hili.

Baada ya vikao vingi vya kukamilisha hili na kupanga jinsi ya kulikamilisha hatimaye siku ikafika na kijana kutoka TMK Wanaume Family kuuwaga rasmi ukapera na kutuletea shemejiiiii.....!!! Ilikuwa siku ya jumamosi baada ya kuchukuwa kifaa jumla, hii ilikuwa katika kanisa la Azania Front jijini Dar es salaam.

Judith Wambura alizaliwa mkoani Shinyanga tarehe 15 jun, 1979 kwa Martha na Lameck Isambua Mbibo ambao ndio wazazi wake. Inasemekana dada jide alianza kuimba akiwa na umri wa miaka saba, alianza kuimba kanisani kama ilivyo kwa wasanii wengi, bi shosti pia ni moja ya wasanii wa bongo flava wanaoishi kwenye ndoa kwa sasa.

Banana Zorro na Suzy Walele wakilishana keki siku ya harusi yao iliyofanyika katika ukumbi wa Msasani Beach Club jijini Dar - es- salaam. Banana pia ni masanii wa bongo flava ambaye amesha sepa kwenye kundi la ukapera.

Na kwa sasa nadhani huyu ndio atakaye fata tunamuombea kila la kheri mungu ampe wepesi katika hilo Amin inshaallah.