Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Thursday, April 22, 2010

AMWIK WATOA MAFUNZO YA HAKI ZA WANAWAKE NA WAJIBU WAO KWA SERIKALI NCHINI KENYA!!


Kina mama wa kabila la Kiturukana wakiwa na nyuso za furaha mara baada ya kupata mafunzo ya haki za wanawake. Chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Kenya (AMWIK) kimekuwa kikitoa mafunzo kwa kutumia Community Radio Listening Group kuwaelimisha wanawake hao ili wajue haki zao na wajibu wao kwa serikali.
(Picha na Anna Nkinda -Kenya)

Kundi kubwa la ngamia wakiwa wanakunywa maji katika mto Chicho Hoko ulioko wilayani Isiolo katika Mkoa wa North Estern nchini Kenya. Ngamia hao wanamilikiwa na wafugaji wa kabila la waborana.Hivi karibuni wilaya hiyo ilikumbwa na ukame uliosababisha kufa kwa mifugo mingi wakiwemo ng’ombe, mbuzi na kondoo lakini ngamia ni wanyama wanaostahimili hali ya ukame.

Mdau Lawrence Mureith akiwa amesimama nje ya moja ya nyumba ya kabila la waturukana ambao ni wafugaji wanaopatikana huko wilayini Isiolo mkoani Kenya.

Watoto wa kabila la kiturukana wakiwa na nyuso za furaha wakati wanapigwa picha.

Kina mama wa kabila la Kiturukana kutoka kundi la ANUPIT wakiwa katika picha ya pamoja na wanachama wa Chama cha waandishi wa habari wanawake nchini Kenya (AMWIK) mara baada ya mafunzo ya haki za wanawake na wajibu wao kwa serikali yanayotelewa na chama hicho kwa kutumia Community Radio Listening Group.

No comments:

Post a Comment