MTOTO wa mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru, Tonny Mwiru amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kisutu, Dar es Salaam, akikabiliwa na mashitaka ya kujipatia Sh milioni 424 kwa njia za udanganyifu.
Inspecta wa polisi, Emma Mkonyi, leo amesoma mashitaka yanayomkabili mtoto huyo wa Mbunge wa Kuteuliwa.
Katika shitaka la kwanza,mshitakiwa Mwiru, kwa kushirikiana na wenzake wasiofahamika, katika tarehe na mahali pasipofahamika jijini Dar es Salaam walikula njama ya kuiibia kampuni ya SCI (TZ) LTD kiasi hicho cha fedha.
Katika shitaka la pili, mshitakiwa alidaiwa kughushi fomu ya benki ya kuhamishia fedha yenye namba E17 ya Agosti 29, 2008.
Kwa mujibu wa Mkonyi, kijana huyo alighushi fomu hiyo kwa nia ya kuonesha kuwa ilikuwa halali na imesainiwa na Ravishankar Rasiman, Mkurugenzi wa kampuni hiyo huku akifahamu si kweli.
Shitaka la tatu, amedaiwa mahakamani kuwa, Agosti 29, 2008, katika benki ya Barclays katika Mtaa wa Ohio, Dar es Salaam aliwasilisha fomu hiyo kwa mfanyakazi wa benki hiyo,Bituni Chiza,huku akifahamu kuwa haikuwa halali.
Imedaiwa pia kuwa,kati ya Septemba na Octoba 2008 katika benki ya CRDB tawi la Kijitonyama, Dar es Salaam mshitakiwa alijipatia Sh 424,458,799.29 kutoka katika akaunti namba 01j014293000 akionyesha kuwa fedha hizo ni halali zimetolewa na kampuni ya SCI (TZ) LMD kwenda kwenye kampuni ya Temm Power Solution.
Mshitakiwa huyo amerudishwa rumande baada ya kukana mashitaka yote na kushindwa kutimiza masharti ya dhamana yaliyomtaka kuwa na wadhamini wawili.
Mwiru pia alitakiwa atoe Sh milioni 10 pamoja na hati ya mali isiyohamishika yenye thamani hiyo.Kesi hiyo itatajwa Agosti 31 mwaka huu.
Hakimu Mkazi, Gabriel Mirumbe, alimuuliza kama Tonny ni mtoto wa Kingunge Ngombale Mwiru,akajibu kuwa Kingunge ni baba yake mzazi.
Habari mbalimbali toka pande za bongo bila kusahau matukio mbalimbali yanayorindima pande zote za dunia
Psquare Ft. J.Martins- E No Easy
Wednesday, August 18, 2010
Tuesday, August 17, 2010
KIBAKA ALA KICHAPO ASUBUHI KWEUPE!

KIBAKA MMOJA AMBAYE JINA LAKE HALIKUPATIKANA MARA MOJA AKIWA AMEPOTEZA FAHAMU KUTOKANA NA KUPEWA KICHAPO CHA KUFA MTU BAADA YA KUMWIBIA MMOJA WA ABIRIA ALIYEKUWA NDANI YA GARI AKIWA AMETOKEA ENEO LA TANDIKA AKIELEKEA MWENGE, KIBAKA HUYO ALIMPORA ABIRIA HUYO SIMU KUPITIA DIRISHANI NDANI YA DARADARA HIVYO WANANCHI WENYE HASIRA WALIMKIMBILIA WAKAMKAMATA NA KUMPA KICHAPO CHA MAWE, ENEO LA KARUME SOKONI ILALA JIJINI DAR ES SALAAM, AMBAPO TUKIO HILO LIMETOKEA JANA SAA NNE ASUBUHI

KIBAKA AKIWA HAJITAMBUI KWA KIPIGO ALICHOKIPATA KUTOKA KWA WANANCHI WENYE HASIRA.
Monday, August 16, 2010
Utafiti global publishers!

Mwandishi Wetu na Mashirika ya Habari
Utafiti wa kisayansi uliofanywa hivi karibuni nchini Marekani na Uingereza kisha kuripotiwa na Jarida la New Study umebainisha kwamba, wanawake wenye matiti makubwa huwasisimua zaidi wanaume kimapenzi kuliko wengine.
Jane Pincott Mwandishi wa masuala ya sayansi amekiri katika kitabu chake cha ‘Do Gentleman Really Prefer Brondes’ kwa kueleza kinagaubaga juu ya utafiti huo kuwa , nguvu ya mvuto wa wanawake wa aina hiyo ni kubwa na kufafanua kwamba ina uwezo mara dufu wa kuteka hisia za wanaume.
“Hakuna mwenye kupinga kuhusu hili, dunia nzima inafahamu na hasa wanaume wenyewe…kigezo cha kwanza cha kumtambua mwanamke ni matiti, …kadiri yanavyokuwa makubwa utambulisho wake hukua na mvuto huongezeka.
“Mwanamke kuwa na sura nzuri peke yake haitoshi…ingawa wanaume hupenda hilo pia, lakini si jambo linaloamsha hisia zao za mapenzi haraka, tumetafiti na kubaini ukweli huu tunaoueleza,” alisema Pincott alipozungumza na New Study.
Timu ya wataalamu iliyoendesha utafiti huo, ilihusisha zaidi ya wanaume 4,000, kwa kuwaweka kwenye chumba chenye picha za wanawake wenye matiti makubwa na madogo, ambapo ilibainika asilimia 79 ya waliotazama picha za wanawake wenye matiti makubwa walisisimka kimapenzi.
Naye Dk. Grazyna Jasienska wa Chuo cha Harvard aliongezea nyama kwenye uchunguzi huo kwa kusema kuwa, mwanamke mwenye matiti makubwa ana uwezo wa kushika ujauzito haraka kuliko aliyenayo madogo.
Ripoti hiyo ya watafiti wa nje inaweza kuwa na ukweli hata kwa wanawake wa kibongo ambao nyakati hizi wamekuwa wakiacha nje sehemu kubwa ya matiti yao makubwa, bila kubainisha sababu wazi za kufanya hivyo.
“Nakubaliana kwa kiasi fulani na utafiti huo kwa sababu za kitaalamu, matiti ni kiungo nyeti chenye hisia za mapenzi, kinapoonekana kwa wazi huvutia, hii haijalishi kama ni matiti ni makubwa au madogo.
“Lakini kwa kuwa matiti makubwa huonekana kirahisi mwanamke anapokuwa amevaa nguo, hiyo inaweza kuwa sababu ya wenye matiti hayo kuvutia,” alisema Richard Manyota mwanasaikolojia mahiri nchini.
Warembo wa kibongo wenye matiti makubwa ambao wamekuwa na tabia ya kuyaweka wazi bila kueleza kama wanatumikia utafiti huu ama la ni pamoja na Aisha Ramadhani ‘Isha Mashauzi’ (pichani), Aunt Ezekiel, Moureen Gislary, Ndumbagwe Misayo ‘Thea’, Fideline Iranga, Rehema Chalamila ‘Ray C’ na wengineo.
Ufafanuzi kuhusu Mwakalebela vs Mramba na Chenge



Baada ya jina la Frederick Mwakalebela kuenguliwa katika orodha ya wagombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi, CCM, baadhi ya watu wamekuwa wakihoji uhalali wa kufanya hivyo il hali wana-CCM wengine wanaogombea viti hivyo katika majimbo mengine nchini wana kesi mahakamani lakini wameruhusiwa kuendelea na kinyang'anyiro hicho. Maswali hayo yaliifikia CCM na hapa ni ufafanuzi wake:Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC-CCM), John Chiligati amesema kesi inayomkabili mshindi wa kura za maoni aliyepokwa ‘haki’ ya kuteuliwa kugombea ubunge wa Iringa Mjini kwa tiketi ya chama hicho, Frederick Mwakalebela, haifanani na washindi wengine wa kura za maoni walioteuliwa ambao ni Basil Mramba anayegombea jimbo la Rombo na Andrew Chenge anayegombea jimbo la Bariadi Mashariki licha ya kuwa na kesi mahakamani kama yeye.
Alisema, Mwakalebela ameachwa kwa sababu kukosa kwake maadili.
“Suala kwa Mwakalebela ni maadili tu, katika mchakato huu, kakamatwa kwa tuhuma za rushwa na TAKUKURU wamesema wanayo sababu ya kumpeleka mahakamani." “Lakini alikuwa ndio kwanza kaingia katika mchezo wenyewe na katika mchezo huu huu kabla ya dakika 90, akapigiwa filimbi kuwa amecheza faulo,” alisema Chiligati.
Kuhusu tofauti ya Mramba, Chenge na Mwakalebela Chiligati alisema, “ kisheria wote ni watuhumiwa na hawakutwa na hatia, lakini kimaadili ni tofauti… Mramba anatuhumiwa kutumia vibaya madaraka, tuliita wanasheria wakasema hiyo kesi haimuondolei sifa ya kuwa mgombea.”
Hata hivyo alikiri kuwa Mramba alipitishwa baada ya kufanyika mjadala kati ya wajumbe hao wa NEC.
“Katika Mkoa wa Shinyanga Jimbo la Bariadi Mashariki aliteuliwa Chenge kutetea nafasi yake, anayo kesi ya trafiki, haimkoseshi haki ya kuwa mgombea,” alisema Chiligati.
Subscribe to:
Posts (Atom)


