Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Tuesday, September 7, 2010

Edward Nino: Mcolombia, mtu mfupi zaidi duniani


Edward Nino Hernandez akiwa na nakala ya kitabu cha kumbukumbu cha Guinness (Guinness World Record Book) baada ya kudai kushikilia rekodi ya mtu mfupi zaidi duniani.

REKODI ya mtu mfupi zaidi duniani inadaiwa kushikiliwa na Edward Nino (24), raia wa Colombia, ambaye ana urefu wa sentimita 70 au inchi 27.

Nino ametambuliwa rasmi na Rekodi za Dunia za Guinness kuwa ni mtu mfupi zaidi duniani baada ya mtu aliyekuwa akishikilia rekodi hiyo, He Pingping, raia wa China, ambaye alifariki mwezi Machi mwaka huu akiwa na urefu wa inchi 22.

Nino, mwenye uzito wa kilo 10 anajifunza kucheza sinema akiigiza kama jambazi “dogo” lenye kuuza madawa ya kulevya lakini likauawa katika mashambulio ya bunduki.

Nino, anayesema anapenda kucheza dansi, hapo nyuma alikuwa akinengua katika baa moja.





Akionyesha umahiri wake katika kucheza dansi huko Bogota ambako anafanya kazi kama kibarua.

Wazazi wake wanasema kaka wa Nino pia ni mfupi, akiwa na inchi 37 tu, lakini kaka zake wengine watatu wana vimo vya kawaida. Wazazi hao walimpoteza binti yao ambaye naye alikuwa na ufupi kama huo mnamo 1992, akiwa bado hajatimiza hata mwaka mmoja tangu azaliwe.

Nino anayetoka eneo la Bosa katika wilaya maskini ya Bogota, ana afya njema japokuwa huwa analalamikia kutoona vizuri. Pia ana rafiki wa kike mwenye umri wa miaka 18 aitwaye Fanny ambaye ana urefu wa futi tano, ambao ni urefu mkubwa sana ukilinganishwa na yeye.

Anasema huwa anajisikia vizuri tu kuhusiana na urefu wake, japokuwa anasema watu saa nyingine humkera kwa kumshikashika.


Akisuburi usafiri nyumbani kwake kwenda kazini.

Matumaini yake ni kutaka amiliki gari aina ya Mercedes (Benz) na kukutana na watu mashuhuri kama Jackie Chan, Sylvester Stallone na rais wa zamani wa Colombia, Alvaro Uribe.

Hata hivyo, rekodi yake hiyo inaweza kuvunjwa karibuni na Khagendra Thapa Magar wa Nepal ambaye ana aurefu wa sentimita 56, akiwa ni kijana mfupi zaidi duniani hadi atakapotimiza miaka 18 Oktoba 14 mwaka huu

Mrisho Mpoto: Watanzania Tunakufa Kwa Roho Chafu!


JUZI hapa nilipata bahati ya kusafiri na Mrisho Mpoto. Safari yetu ilianzia Iringa kwenda Njombe. Tulikuwa na saa tatu pamoja kujadili masuala juu ya jamii yetu.

Mpoto ni mmoja wa wasanii mahiri na maarufu sana nchini kwa sasa. Na kwangu mimi, Mpoto ni mwanafalsafa anayeifikia jamii pana kwa tungo zake zenye kufikirisha.

Tulipofika eneo la Nyororo, Mufindi, Mpoto alishuka kwenye gari ili tununue chupa ya maji ya kunywa. Ndani ya dakika tatu tukawa tumezungukwa na watu wasiopungua 50. Wote walitaka kumwona Mpoto na kuzungumza naye. Sauti za ’ Mjomba, Mjomba!” zilisikika zikiita.

Tuliondoka mahali hapo baada ya yeye kupiga picha ya pamoja na mashabiki wake. Baadaye alinitamkia; ” Hawa ndio watu wangu, leo wananikubali kwa kuwa nawasemea. Siku nikiacha kuwasemea, watapatwa na huzuni. Watanikataa, nami sitakuwa mtu mwenye furaha pia”. Hapo tukajikita katika kujadili maana ya msanii au mwandishi kuwa kioo cha jamii.

Baadaye kwenye mazungumzo yetu niligusia kauli ya Mpoto kwenye moja ya matangazo ya kijamii redioni. Kwenye tangazo hilo anatamka; ” Kwenda huko, utakufa kwa roho yako mbaya!”.

Nilimwuliza Mpoto swali la kifalsafa; ”Je, binadamu tunakufa kwa roho mbaya au roho chafu?”

”Kaka Maggid, naiona mantiki ya swali lako. Kama nitakunjua viganja vyangu na kuitema roho yangu kisha nikaiangalia… lakini fafanua kwanza fikra zako,” alijibu Mpoto.

Nikafafanua, kuwa binadamu hatukuumbwa kuwa wengine wana roho mbaya na wengine nzuri. Sote tumeumbwa na roho nzuri isipokuwa mazingira ndiyo yanayotufanya wengine tukawa na roho chafu na wengine roho safi. Ndiyo, roho nzuri tulizoumbwa nazo zinachafuka. Tunakuwa ni binadamu wenye roho chafu. Na hakika, Watanzania wengi tunakufa kutokana na roho chafu, zetu wenyewe au za wenzetu.
”Mh!” Anaguna Mpoto. Ananiacha niendelee.

Maana, ni mtu mwenye roho chafu tu anayeweza kuhujumu mradi wa kuangamiza malaria inayosababisha vifo vya maelfu ya watoto na watu wazima kwa tamaa zake binafsi. Ndiyo, kuhujumu mradi wa kuzuia malaria ili apate fedha za kufanya mambo ya fahari au hata kununua uongozi wa kisiasa. Kwa mwanadamu, ni heri ufe kwa kupambana na anayehujumu mradi wa kuangamiza malaria kuliko kufa kwa malaria inayotokana na mbu anayesababisha malaria.”

Tukazidi kuzama kwenye la fikra. ”E bwana, Makambako hapa. Nafurahi kila ninapokuwa mbali na Dar es Salaam,” anatamka Mpoto.

”Kwanini unafurahi kuwa mbali na Dar?” Namwuliza Mpoto.

”Maggid, angalia nje. Hawa ndio Watanzania wanaopambana kila kukicha kwa maendeleo ya nchi yetu na kuna wachache mijini wanaodhani kuwa ni haki yao Watanzania hawa kuishi katika hali ya ufukara pamoja na rasilimali zote hizi tulizonazo.”

Kwa hiyo ndio maana umefurahi kuwa mbali na Dar?”

”Wakati mwingine ni muhimu kutoka nje ya miji mikubwa kama Dar, kwenda mbali na kuona hali halisi,” ananijibu Mpoto.

Turudi kwenye mada ya Watanzania na roho zetu chafu. Na hili lina mantiki katika kipindi hiki cha kampeni za Uchaguzi Mkuu. Nilimsimulia Mpoto kisa nilichopata kukisimulia huko nyuma. Kisa cha bwana aliyemwomba sana Mungu amsaidie. Siku moja akaambiwa; sala zako zimekwishakusikilizwa, isipokuwa, Mungu atakusaidia kwa sharti moja; kwamba kile atakachokupa wewe, basi, jirani yako atampa mara mbili yake.

Bwana yule akahitaji muda wa kwenda kutafakari kabla hajampa Mungu jibu. Akarudi na jibu; ” E Mola wangu, naomba unipe chongo, utoboe jicho langu moja. Bwana yule alikuwa tayari awe na chongo ili jirani yake awe kipofu kabisa!

Na hakika, Watanzania wa kawaida walio wengi si watu wenye roho chafu. Isipokuwa, tuna bahati mbaya ya kuwa na baadhi ya viongozi wabinafsi na wenye roho chafu huku wakilindwa na mapungufu ya kimfumo katika matendo yao maovu.

Ni viongozi ambao, kama kuna kuchagua kati ya wao kupata kimoja na wanaowaongoza kupata viwili, basi, wana hiari ya kuchagua kupata kilema cha mguu mmoja ili wanaowaongoza wawe viwete.

Ndani ya roho ya mgombea hana chema anachowatakia wapiga kura wake. Anajiangalia yeye tu. Yote hii inatokana na kukithiri kwa ubinafsi. Na mapungufu ya kimfumo nayo yanawasaidia viongozi hawa wabinafsi kutenda maovu yao kwa wananchi bila hofu. Katika kuendekeza ubinafsi wao, unaweza kabisa kuamini, kuwa viongozi hawa wanawachukia Watanzania wenzao.

Ni kwa sababu ya ubinafsi na roho zao chafu. Na anachoshindwa kuelewa kiongozi huyu anayechukia maendeleo ya mpiga kura wake ni ukweli kuwa maendeleo ya mtu huyo binafsi yatakuja kwa namna moja au nyingine kumnufaisha hata yeye na Taifa kwa ujumla. Na tuna wabunge wengi watakaoangushwa na wapiga kura wao katika uchaguzi wa Oktoba kwa sababu wameshindwa hata kuficha makucha yao ya ubinafsi.

Kwa wabunge hawa, miaka mitano ya kukaa bungeni imewaletea neema kubwa wao binafsi huku majimbo yao bado yakiwa nyuma sana kimaendeleo. Lakini, kuna wabunge ambao, wamejitahidi sana. Na mifano ya juhudi zao za kuwaletea maendeleo watu wa majimbo yao inaonekana.

Hawa watatendewa haki, maana, wananchi wa majimbo husika wanawajua na wanajua waliyoyafanya kwa maendeleo ya majimbo yao. Hakika, wananchi wamechoka kuvutwa nyuma kimaendeleo. Kuvutwa nyuma kunakosababishwa na baadhi ya viongozi waliowapa dhamana za uongozi.

Mathalan, katika nchi hii hutokea anayehusika na kuwasaidia Watanzania wenzake kupata nafasi za kwenda kusoma nje ya nchi akatoa nafasi hizo kwa upendeleo. Ataanza na familia yake, ndugu na atamalizia na jamaa na rafiki zake. Wakisha hao yuko tayari nafasi hizo zibaki tupu kuliko kuwasaidia Watanzania wengine.

Kuna vyuo vya humu duniani utakuta wamejaa Waafrika kutoka nchi nyingine, iwe Ghana, Nigeria, Kenya na kwingineko. Lakini utashangaa ni kwa nini idadi ya Watanzania ni ndogo sana au hawako kabisa kwenye vyuo hivyo. Tofauti hapa ni ukweli kuwa wenzetu katika mataifa mengine wanasaidiana sana katika kupashana taarifa juu ya kuwapo kwa vyuo hivi na namna ya kupata nafasi hizo. Mathalan, nchi kama Ghana ikitengewa nafasi 50 kwa mwaka katika vyuo vya nchi ya kigeni, basi idara husika katika Ghana itahakikisha nafasi hizi zinajazwa.

Tuna haja ya kufanya jambo moja muhimu kwa sasa; tujenge moyo wa uzalendo na utaifa. Tuipende nchi yetu. Tupendane kama Watanzania. Ubinafsi uliokithiri na kuwa na roho chafu, hususan, kwa baadhi ya tuliowapa dhamana za uongozi unatuweka mahala pabaya kama Taifa. Huko tunakokwenda tatizo hili litatutafuna. Ndiyo, roho zetu chafu zitasababisha Taifa kuangamia. Mtaona ishara…

POLE SANA MR NICE



Jana mwenye nyumba wa Mr Nice alimpigia simu Gea Habib aende akamsikilize Nice maana kuna matatizo yanayomkabili.Basi Gea akaenda huko Mwananyamala kwa manjunju na mama mwenye nyumba kumuita Nice wakakaa kuzungumza...Gea anasema Mr.Nice alikuja akichechemea akitokea chumbani.

Nice akaeleza kuwa juzi kulitokea ogomvi kati ya mpenzi wake na ndugu zake yeye akiwa ndani anawasikiliza na katika ugomvi huo ndugu walikuwa wakimtuhumu mpenzi wa Nice kuwa siku hizi anawabagua kisa yupo na Nice.Nice aliposikia jina lake likitajwa akatoka nje akawaambia ndugu hao waache kutaja jina lake yaani wasimuhusishe katika ugomvi wao.Baadae ugomvi huo ukaisha na kila mmoja kutawanyika.


Ilipofika usiku saa tatu ikaja gari na wakaka wawili na mmoja wa ndugu wa yule mpenzi wa Nice anaitwa Zulfa wakamuita Nice wakajitambulisha wao ni police na wamepokea malalamiko kutoka kwa huyo dada kuwa kampiga na wamekuja kumkamata.


Wakamuonyesha RB ya yule dada na Nice akaamriwa atoke ili aende kituoni kulikopelekwa malalamiko.Nice hakubisha akaondoka nao kwenye gari yao ndani ya gari wakamwambia wao sio polisi wala nini ila watamkomesha basi wakamfunga kitambaa usoni,wakampiga sana na kumsababishia majeraha.

Baaada ya kipigo wakamuita jamaa yao mwingine aje na kamera anasema wakamvua nguo na kumpiga picha akiwa mtupu..wakamfungua kile kitambaa walichomfunga usoni wakamlazimisha aiangalie kamera wakampiga picha nyingi sana.


Wale watu wakamwambia una bahati una Ukimwi la sivyo tungekufanyia mambo makubwa zaidi ya hayo.Na wakati wanampiga wakawa wanaambiana msimtoe damu maana mkimgusa mtaambukizwa Ukimwi.

Nice akaendelea kuelezea kuwa toka saa tatu usiku walipomchukua mpaka saa nane ndio wamekuja kumtupa uwanjani Temeke huko akiwa mtupu na nguo wakamtupia pembeni. Walipoondoka ndio na yeye kutoa kitambaa machoni akavaa nguo zake na kuomba msaada wa usafiri wa tax maana hakuwa na hela wala simu.

Nice akarudi mwananyamala na kwenda kutoa taarifa polisi na polisi jana wakafanikiwa kumkamata huyo dada ili aeleze wale watu ni kina nani na kwa nini wamefanya vile.Nice alilia sana na akasema hajapendezwa na kitendo alichofanyiwa kwani kinamuuma na kummsononesha sana
Jamani mie sielewi Mr.Nice amekuwa akiandamwa na zimwi la kupigwa pigwa kila siku sijui kwa nini

Monday, September 6, 2010

NI MIPANGILIO TU CHOCHOTE KINAWEZEKANA!



Beautifuly the Big name & Big Body from Maisha Plus season one Efrancyia akiwa Kwenye pozi zito



Akijaribu kulekebisha nywele zake


...... akijaribu kumbebarafiki yake kipenzi Moshi

DAKA HII MDAU WANGU ANATAFUTA BWANA KAZI KWENU WADAU!


Huyu mtoto ni hot n’ sexy kiasi cha kumtoa nyoka kwenye shimo lake, anakwenda kwa jina la Moshi Mahona (23), aliwahi kushiriki katika Kijiji cha Maisha Plus, Season 0ne, anapatikana Mitaa ya Sinza, White-Inn Dar, in short sistaduu huyu anatafuta mchumba atakayemuoa na kwamba yuko tayari ku-testiwa kwa sharti moja tu, kupima ngoma kwanza. If u need to have dat chick…..plz use 0754-557440 or 0712-956910. watch out to UMBEABONGO.COM, mizigo kama hii iko ya kumwaga na tutakuletea mara kwa mara!!!

AKU SIMO MIE NI POZI TU LA PICHA!!

pombe si chai jamani