Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Saturday, February 27, 2010

ONYO KWA WATUMIAJI WA DAWA ZA KICHINA KUONGEZA MAKALIO




Tukio la karibuni la kijana Gasper Honza, mkazi wa Mbezi Juu, jijini Dar es Salaam, mengi yameibuka baada ya kuelezwa kuwa, nyeti hiyo inazidi kukua.

Bado imesisitizwa kwamba, kukosewa kwa dozi ya ‘hipson’ ambayo ni maalum kwa ajili ya kukuzia makali ndiyo chanzo cha nyeti hiyo kugeuka ‘zigo’ la kilo 10.

Katika tukio hilo, Honza alikaririwa na gazeti moja la kila siku akielezea mkasa mzima kuwa alifanya uamuzi huo baada ya kutelekezwa na wanawake watatu kutokana na tatizo hilo, hivyo alitaka kuinusuru ndoa yake na mke wa nne.
Alisema kuwa, alitumia dawa hizo baada ya kupata ushauri kutoka kwa rafiki yake wa karibu aliyemtaja kwa jina la Sebastian Mkwema ambaye aliwahi kuwa na tatizo kama hilo.

“Mkwema aliniambia nimpe elfu 30 ili kupata dawa ya kukuza nyeti zangu, siku tatu baadaye aliniletea, nilianza kupaka na kuona nyeti zikiongezeka, nilipata furaha ya kuinusuru ndoa yangu.

“Kwa bahati mbaya nilikosea masharti, ilikuwa nipake kwa muda wa siku mbili tu, mimi nilitumia wiki nzima ambapo matokeo yake ni kama unavyoona sasa (huku akionesha nyeti zake) ni mzigo mkubwa, hata suruali sivai na tendo la ndoa sifanyi.
“Kazi nilishaacha tangu Septemba mosi, mwaka jana,” alinukuliwa.

Kwa upande wake, mke wa Honza, Nancy Kilungi, ambaye alimtelekeza mumewe baada ya nyeti hizo kuvimba alinukuliwa akisema: “Ndugu yangu ndoa ni unyumba …nitaishije? Hakuniambia tatizo lake tangu awali na alishakimbiwa na wake watatu, mimi ni wa nne.

“Alikuwa na ‘mashine’ ndogo kama kidole kidogo cha mkononi, tulishahangaika sana hadi kwa waganga wa kienyeji bila mafanikio,” alisema.

Ilielezwa kwamba, Mkwema ambaye kwa sasa amehamia visiwani Zanzibar, alikiri kumshauri Honza kutumia dawa hiyo ambayo alidai yeye ilimsaidia na sasa ndoa yake ina amani: “Hee ndoa yangu ilikuwa inawaka moto. Mke wangu alikuwa anataka talaka, nilikosa usingizi, lakini Mungu si Athuman… jamaa fulani alinishauri kutumia ‘hypson’ na sasa mambo si mabaya.”

Kwa upande wa familia ya Honza walisema jambo hilo ni la kusikitisha kwani amepoteza uwezo wa kufanya kazi na amekuwa mtu wa kukaa nyumbani tu.

“Yale yale ya akina Michael Jackson. Mungu anakuumba hivi, wewe unataka hivi na vile… tunafanya utaratibu wa kupata matibabu,” alisema mmoja wa wanafamilia hao.

Risasi lilipopiga simu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, mmoja wa watu aliyejitambulisha kwa jina la John Rumisha alitoa onyo kali kwa wale wanaopendelea kutumia dawa za kubadili maumbile kwani madhara yake ni makubwa zaidi ukilinganisha na gharama za dawa hizo.

Alisema kuwa, kumekuwa na ongezeko la watanzania wanaotumia dawa za Kichina kuongeza viungo mbalimbali vya mwili, lakini madhara yake ni makubwa kuliko mtu angeamua kuishi kama alivyoumbwa.

Wiki kadhaa zilizokatika, gazeti ndugu na hili, Ijumaa liliripoti habari ya mwanamke aliyekuwa akilalamika kuteswa na makalio ya Kichina ambaye alilenga kukuza ‘hips’ zake, lakini baadaye alijikuta akiharibika vibaya mwili wake.

Katika siku tulizonazo kumeibuka dawa ambazo zinaelezwa kuwa ni za Kichina ambazo baadhi ya watu waliopata kuzitumia wamekuwa wakikiri kupata madhara makubwa kama vile ‘kalio’ moja kuwa kubwa kuliko jingine, kujazia zaidi chini kuliko juu na mwili kufa ganzi.

No comments:

Post a Comment