Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, August 13, 2010

BRAZAMEN ACHANGAMKIA UKOKO WA PILAU KWENYE MAULID


Brazamen Haji (kushoto) akiwa anapakuliwa pilau ambalo baadaye lilitua kwenye Rambo lake.
Na Dunstan Shekidele, Morogoro
KIJANA mmoja smati aliyefahamika kwa jina moja la Haji mkazi wa maeneo ya Nunge mjini hapa, aliwashangaza watu waliohudhuria sherehe ya Maulid ya kumtoa mtoto kufuatia kitendo chake cha kwenda jikoni akiwa na mfuko wa ‘Rambo’ na kuomba atiliwe pilau pamoja na matandu yake ili aende navyo nyumbani kama “take away”.

Paparazi wetu ambaye alikuwa mmoja wa waalikwa mashuhuri hapo alistaajabu kuona kundi la kina mama wakiangua kicheko baada ya kumwona Brazamen huyo akichomoa mfuko wake wa Rambo aliokuwa ameuhifadhi kwenye ‘jeans’ lake na kuomba atiliwe pilau hilo kwenye mfuko huo.

Kijana huyo ambaye alikata mshipa wa aibu alipofika kwenye sufulia la pilau hilo, alimshawishi mpishi amjazie msosi, na mpishi huyo baada ya kuona macho mengi ya watu yakielekezwa kwake, aliamua kutumia ‘Uislamu’ na kumjazia Braza huyo pilau kama wanavyoonekana pichani.

No comments:

Post a Comment