Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Monday, September 6, 2010

Hali ni shwari Msumbiji baada ya ghasia



Taarifa kutoka Msumbiji zinasema sehemu kubwa katika mji mkuu, Maputo, kwa sasa ni shwari baada ya ghasia za wiki iliyopita ambazo zilisababisha watu kumi kufariki na wengine takriban mia tatu kujeruhiwa.

Ghasia hizo zilitokana na maandamano ya kupinga kupanda kwa bei ya mkate na bidhaa nyinginezo kwa kiwango kikubwa.

Katika baadhi ya matukio, polisi walitumia risasi za mpira dhidi ya waandamanaji.

Msemaji wa Shirika la Msalaba Mwekundu katika mji mkuu, Americo Ubisse, alisema kuna wasiwasi wa ghasia kuzuka tena siku ya Jumatatu, wakati ujumbe wa simu za mkononi ukisambazwa kwa watu ili wafanye mgomo

Ujumbe kama huo ulitumiwa kabla ya kuzuka kwa ghasia za juma lililopita.

No comments:

Post a Comment