Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Tuesday, September 7, 2010

Upendo Nkone Kufunga Ndoa Tarehe 17 October 2010


Muimbaji wa Injili Upendo Nkone atategemea Kufunga ndoa tarehe 17 October 2010 na Mchungaji John Mbeyela ambaye pia ni mjane mwenye watoto watatu, ndoa hiyo itafungwa katika kanisa la Naioth kwa Mchungaji Mwasota.
Akiongea na Strictly Gospel Upendo Anasema “Ninafurahi sana na ninaomba Mungu akamfute machozi kila mjane, haijalishi umekaa miaka mingapi. Mungu yupo atakukumbuka”
Bi. Nkone ambaye ameishi maisha ya ujane kwa miaka 9, ana jumla ya album tatu ambazo ni Mungu Baba, Hapa Nilipo na Zipo faida.
Tunamtakia kila la heri katika maandalizi yote mpaka harusi

No comments:

Post a Comment