Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, September 8, 2010

CHADEMA yaazimia kuishitaki CCM kwa Wapiga Kura


L-R: Mabere Marando | Prof. Mwesiga Baregu | John Mnyika
Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Kampeni ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Prof. Mwesiga Baregu akiwa na viongozi wengine wa chama hicho, leo katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam amezungumzia maamuzi ya Msajili wa Vyama vya siasa nchini kutupilia mbali malalamiko ya chama hicho dhidi ya mgombea wa Uraisi kupitia CCM, Jakaya Kikwete.

Amesema CHADEMA imeweka wazi kuwa haitaweza kwenda mahakamani kutaka mgombea Uraise kupitia CCM, Jakaya Kikwete, aenguliwe kushiriki uchaguzi na badala yake watawashawishi wananchi wasimpigie kura mgombea huyo wa CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Uamuzi CHADEMA unakuja baada ya wakili wa chama hicho ambaye pia ni mjumbe wa timu ya Taifa ya kuratibu kampeni za uchaguzi, Mabere Marando, kutoa ushauri wa aina mbili ambao ni, kwenda Mahakama kuu kuomba marejeo ya maamuzi ya Tendwa ili mahakama hiyo itoe maamuzi ya haraka ya kumuondoka Rais Kikwete kugombea Uraisi au; Kushitaki kwa kutumia sheria ya gharanma za uchaguzi.


credit source: http://www.wavuti.com/habari.html#ixzz0yvXkVguQ

No comments:

Post a Comment