Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Sunday, June 13, 2010

Benki ya Dunia kuimwagia Bongo mkopo wa Mil. 914,200!


Kuanzia sasa itaanza kupokea Mkopo wa Sh. milioni 914,200 kutoka ndani ya Benki ya Dunia (WB), kwa madhumuni ya miradi mitano, mipya mitatu ikiwemo na mingine miwili.

Kwani utiaji saini wa mkopo huo ulifanywa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhani Khijjah na Mkurugenzi Mkazi anayewakilisha benki hiyo katika nchi za Tanzania, Uganda na Burundi, John Murray McIntire katika hafla iliyofanyika mjini hapa jana.

Na miradi mitatu mipya itakayogharimiwa na fedha hizo ni pamoja na Awamu ya Pili ya Mpango wa Maendeleo ya Elimu, Mradi wa Kusaidia Sekta ya Usafirishaji na Mradi wa Kuboresha Miji.

Kwani miradi hiyo mitatu jumla imepewa takriban Sh. milioni 816,000.

Na Miradi inayoendelea iliyopata mkopo huo ni ule wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) na Mpango wa Maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) ambayo kwa pamoja ilipata Sh. milioni 49,280.

Mbali na miradi hiyo..pia mradi wa Elimu ya Sekondari una lengo la kuboresha miundombinu ya shule, walimu na ufundishaji wa masomo ya Hesabu, Sayansi na Lugha pamoja na kuziongozea uwezo wa kifedha na utalaamu shule.

Kuhusu mkopo kwa ajili ya Mradi wa Usafirishaji, utasaidia kuboresha barabara kadhaa nchini vikiwemo na viwanja vya ndege.

Baadhi ya barabara ambazo alisema zitakarabatiwa kwa fedha hizo ni ile ya Korogwe- Same na ya Arusha hadi Minjingu.

Pia viwanja vya ndege vitakavyofaidika na pesa hizo ni vya Tabora, Kigoma na Bukoba.

Kuhusu mradi wa kuboresha miji, miji itakayofaidika na fedha hizo kuwa ni Mwanza, Arusha, Mbeya, Mtwara, Kigoma na Dodoma.

Na lengo kubwa la mradi huu ni kuboresha miji hii na hususan kuboresha huduma mbalimbali mijini, hususan upanuzi wa barabara.

No comments:

Post a Comment