Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, June 11, 2010

Soko la nyama nchini laelezwa kuimarika


Soko la nyama ya ngombe nchini limeelezwa kukua kwa kasi nzuri, kutokana na kuuza nje ya nchi kati ya tani 6 na 10, kiwango ambacho hakikuwahi kuuzwa katika kipindi cha nyuma.

Akielezea mafanikio hayo, Afisa mauzo wa Bodi ya nyama nchini Kaiza Kuwana amesema soko la ndani na nje ya nchi kwa sasa ni kubwa kwa bidhaa hiyo, na kwamba juhudi zinafanyika kuuza wanyama wetu katika nchi ya Kenya kwa njia sahihi zitakazoingiza fedha za kigeni kwa Taifa, tofauti na inavyofanyika kimagendo kwa sasa.

Amesema kilo moja ya nyama inauzwa hadi Dola 4.25 za Kimarekani, na kwamba iwapo uzalishaji utaendelea kuborewshwa, nchi itazidi kunufaika.

No comments:

Post a Comment