Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, June 11, 2010

Twanga kuazimisha Miaka Kumi!


Wazee wa Kisigino Twanga Pepeta bendi maarufu sana na ya muda mrefu inatarajia kutimiza miaka 10 toka kuanzishwa kwake kwa style ya kipekee ndani ya uwanja wao wa nyumbani pale Leaders Club.

Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka “Jiwe” alisema kuwa pamoja na kusheherekea miaka hiyo Kumi lakini pia kutakuwa na uzinduzi wa album yao mpya na ya Kumi pia inayojulikana kama “Mwana Dar es Salaam”

“Kutakuwa na maandamano ambayo yataanzia ofisi zetu zilizopo Kinondoni mpaka viwanja vya Leaders ambako kutakuwa na bonanza ambalo litakuwa na michezo mbalimbali kuanzia kuvuta kamba, mbio za kuku, mpira wa wavu kwa wanawake, mpira wa miguu na zaidi ya hilo kutakuwa na burudani mbalimbali za wasanii wa kibongo na nje ya bongo ambao watasindikiza sherehe hizo” alisema Asha Baraka.

No comments:

Post a Comment