Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, June 9, 2010

TUCTA acheni kutudanganya, sie watu wazima jamani!!


Vyanzo vya kuaminika vinanyunyiza kwamba eti...shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), linacheza usanii wa kipolitiki baada ya juzi kutoa tamko la kuipa serikali ya JK siku saba kuanzia juzi iwe imepandisha mishahara ya wapigakazi au itaitisha upya mgomo wa nchi nzima.

Wadadisi wanadai kuwa wamegundua mkwara huo ni wa kisiasa kwa ajili ya kuwapiga changa la macho wafanyakazi ili waonekane wana ubavu wakati ukweli unabaki palepale kuwa tayari yapo makubaliano tangu Mei 8, mwaka huu ya kupandisha mishahara.

Kwa mujibu wa vyanzo vya uhakika, Tucta na Serikali walifikia makubaliano hayo kuwa serikali iongeze mishahara hiyo na hilo litatelezwa katika bajeti ijayo ya serikali itakayosomwa bungeni Dodoma Alhamisi wiki hii.

“Makubaliano yamefanyika kati ya Tucta na Serikali kuhusiana na masuala hayo ya mishahara ya wafanyakazi".

" Kimsingi ni kuwa wamekubaliana kuwa mishahara mipya itatangazwa katika bajeti ijayo ambayo itasomwa Juni kumi…sasa hawa wanacheza mchezo wa usanii wa kisiasa,” kilieleza chanzo chetu na kuongeza: “Wanafanya hivyo kwa sababu wanajua ndani ya siku hizo saba, serikali itasoma bajeti yake na mishahara itapandishwa na serikali, hivyo wanataka watambe kwa wafanyakazi kwamba ‘mmeona serikali imesalimu amri, ipandishe mishahara’ wakati haya ni makubaliano ya tangu Mei nane mwaka huu.

No comments:

Post a Comment