Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, June 9, 2010

MwanaCCM azua tafrani msibani!


Katika hali ya kushangaza huku wengi wetu tukiamini hali imeanza kuwa tight miongoni mwa politicians wa hapa bongo hususan kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu.

Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Mpanda mkoani Rukwa, amesababisha mtafaruku msibani baada ya kutangaza nia yake ya kugombea udiwani katika msiba wa ndugu yake ambaye ni mmoja wa wazee maarufu mjini humo.

Tukio hilo limetokea juzi mchana katika Mtaa wa Mji wa zamani katika Kata ya Kashaulili wakati waombolezaji wa msiba wa marehemu Matwiri Igembesao walipokuwa wanatangaziwa utaratibu wa jinsi ya msiba utakavyoombolezwa.

Ndipo mgombea huyo aliyetambuliwa kama Salumu Mbegele alipokwenda kushika kipaza sauti na kutangaza nia yake ya kugombea udiwani kwa tiketi ya CCM, Kata ya Kashaulili mbele ya Meya wa Mji wa Mpanda, Yasssin Kantampa ambaye pia ni Diwani wa Kashaulili.

Mbegele alisema yeye ni mzaliwa wa Mpanda kwa hiyo anatumia haki yake ya kikatiba kugombea nafasi hiyo ya kisiasa katani humo na alitumia fursa hiyo kuwaomba waombolezaji hususani wanachama wa CCM watakaoshiriki kupiga kura za maoni basi wamchague ili awatumikie katika kutatua matatizo yao ya kijamii ambayo ni kero kwao.

Baada ya Mbegele kutangaza nia yake hiyo, waombolezaji walianza kuondoka msibani hapo kwa hasira huku wakiguna na kudai pale msibani hapakuwa mahali pa kutangazia nia ya kugombea udiwani.

No comments:

Post a Comment