Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, June 18, 2010

FEDHA ZA SERIKALI ZITUMIKE KWA MALENGO!!


Wabunge wameishauri Serikali kutumia vizuri fedha za barabara ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa fedha zote zinazopelekwa Wilayani kwa ajili ya ujenzi wa barabara zinatumika kwa utaratibu uliopangwa.

Wakichangia hotuba ya Waziri Mkuu Wabunge hao pia wameiomba Serikali kutoa mafungu ya fedha mikoani kwa uwiano unaoweza kuwasaidia wananchi.

Akitoa mchango wake, Mbunge wa Lindi Viti Maalum, Mhe. Riziki Said Lulida amesema, Serikali haina budi kuwa macho na watu wanaoingia hapa nchini kwa kivuli cha wawekezaji kwani wengine huja nchini hata bila mtaji wa kutosha badala yake waletwe wawekezaji wenye uwezo wa uwekezaji.

Mbunge wa Mafia, Mhe. Abdulkarim Shah ameitaka Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Uvuvi na Mifugo kuweka utaratibu wa kuwapatia wavuvi nyezo bora katika shguhuli ya uvuvi ili kuinua kiwango chao katika uvuvi.

Wabunge hao pia wameitaka Serikali kuendelea na utaratibu wake wa kutoa mbolea ya ruzuku kwa wakati kwa nchi nzima ili mkulima aweze kuongeza uzalishaji na tija

No comments:

Post a Comment