Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, June 9, 2010

Eti CCJ kuungana na CHADEMA??


Wakati ile sinema ya kuigiza ikiendelea kati ya Chama cha Jamii CCJ na msajili wa vyama vya siasa..kuhusiana na utata wa usajili wa kudumu wa chama hicho.

Mabosi wa chama hicho..kana kwamba wameshaanza kusoma alama za nyakati..kuwa hawana lao kwa uchaguzi wa mwaka...kitendo kilichowafanya waamke gizani hapo jana na kutangazia wafuasi wake waiunge mkono Chadema kama msajili huyo hatawapa kabisa usajili wa kushiriki uchaguzi wa Oktoba.

Kauli hiyo ya kustua ya CCJ kutangazia wafuasi wake kuunga mkono Chadema inakuja kipindi ambacho chama hicho kimetangaza kufungua kesi mahakamani kutaka uhakiki wa wanachama wake usitishwe kwa tuhuma za kukiukwa taratibu.

Naibu Katiba Mkuu wa CCJ Dickson Ng'hily, alitangaza hilo kwa kutaka Watanzania kuunga mkono Chadema kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba kwani lengo la kuanzishwa chama hicho ni kuiondoa CCM madarakani.

Ng'hily ambaye kiongozi ni msaidizi wa mtendaji mkuu wa chama, alitoa kauli hiyo wakati wa matembeza ya amani yaliyoandaliwa na Chadema, maalumu kwa ajili ya kurudisha fomu kwa wanachama wanaotaka kuwania nafasi za ubunge na udiwani kwa jimbo la Ubungo.

“Wakati tunaanzisha CCJ tuliwaambia CCM kuwa watanzania wamechoka na wanataka mabadiliko, kwakuwa lengo kuu la CCJ ni kuleta mabadiliko niwaombe watanzania kuunga mkono Chadema kwani sera zake zimeonyesha dhamira ya kweli ya kufikia huko,”alifafanua Ng'hily

Aliongeza kwamba, kauli mbiu ya Chadema kwamba, ‘‘hakuna kulala hadi kieleweke inaonyesha wazi kuwa wanachama hao na viongozi wao wamejitoa mhanga kwa ajili ya kutetea rasilimali za watanzania.’’

No comments:

Post a Comment