Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Sunday, June 13, 2010

Mandela kamata jezi yako!!


Siku ya jana waliweza kumtembelea Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, na kuweza kumpa Jezi ya Ureno yenye jina la Mandela mgongoni.

Si wengine bali ni wale Winga wa Ureno Cristiano Ronaldo na Kocha Carlos Queiroz ndiyo walimtembelea Mandela nyumbani kwake na kwenda mpatia jezi hiyo.

Kwani Ronaldo na Queiroz walikuwa na nafasi ya kuzungumza na Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini, ni mara baada ya mwaliko binafsi kutoka kwa Rais huyo nyumbani kwake mjini Johannesburg.

Na walikuwa na furaha pia ya kumpatia fulana ya jezi ya Ureno, yenye jina la Mandela mgongoni na Na. 91, inayotaja umri wa mkongwe huyo.

Mandela anatimiza umri wa miaka 92 msimu ujao, na afya yake inazidi kudhoofika na anatokea mara chache hadharani.

No comments:

Post a Comment