Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, June 9, 2010

Mamba aonekana maeneo ya Kinondoni!!


Mnyama pori aina ya mamba anayeishi majini, amepatikana katika bwawa dogo lililoko katika eneo la mpaka kati ya mtaa wa Kumbukumbu Block 41 na ule wa ADA Estate kata ya Kinondoni, suala lililozua wasiwasi kwa baadhi ya wakazi katika eneo hilo.

Kwa nyakati tofauti wakazi wa jirani na eneo la Bwawa hilo, wameeleza kuwa mnyama huyo si wa kwanza na kwamba alishapatikana tena mwingine kaika kipindi cha nyuma na walipotoa taarifa kwa idara za mali asili, mnyama huyo alichukuliwa na kuhamishwa, lakini siku za karibuni ameonekana tena mwingine.

Naye Mwenyekiti wa Mtaa wa Kumbukumbu Block 41 Majeshi Shabani amethibitisha kuwepo kwa taarifa hizo, na kueleza kuwa mbioni kuliripoti suala hilo kwa watu wa Mali asili ili kumuondoa.

Amesema ni vyema kuchukua tahadhari mapema kabla ya athari, na hasa kwa kuzingatia kuwa ni kinyume na utaratibu na ni hatari kwa wanyama kama hao kuishi katikati ya makazi ya watu ndani ya eneo la jiji.

No comments:

Post a Comment