Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, June 11, 2010

Kombe la Dunia laanza Kwa Majonzi!!


Kitukuu wa Nelson Mandela Zenani Mandela amefariki dunia.

Afisi ya uhusiano mema katika wakfu wa Nelson Mandela imesema kuwa msichana huyo wa miaka 13 alifariki katika ajali ya barabarani iliyompata hapo jana akiwa njiani kutoka sherehe za mkesha wa kombe la dunia mjini Soweto.

Duru za polisi zimesema uwa dereva aliyesababisha ajali hiyo amekamatwa.

Huku hayo yakiarifiwa, mechi ya kwanza kabisa ya kombe la dunia kuwahi kufanyika barani Afrika inatazamiwa kuanza wakati wowote kati ya wenyeji Afrika Kusini na Mexico.

Timu 32 zinachuana kuwania kombe hilo baada ya mwezi mmoja na aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela anatarajiwa kuhudhuria sherehe ya ufunguzi leo jioni.

No comments:

Post a Comment