Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, June 11, 2010

Ukarabati barabara za jiji wapamba moto



Zoezi la ukarabati wa maeneo yenye kasoro katika barabara za jiji la Dar es Salaam limeendelea kupamba moto katika Wilaya ya Kinondoni, ambapo leo shughuli za kuziba viraka chakavu vya lami katika barabara ya Sinza Makaburini ilifanyika.

Akielezea maendeleo ya zoezi hilo, msimamizi wa ujenzi huo Immam Mvungi amesema shughuli inayofanyika ni kuvunja sehemu zilizoharibika na kuweka vipande vipya, kupanua maeneo finyu ya barabara pamoja na kuzibua mifereji iliyoziba katika barabara hizo.

Aidha ameeleza kuwa lengo la hayo yote ni kuimarisha barabara hizo ili kuweza kuondoa msongamano wa magari, pale yanapolazimika kupunguza mwendo kutokana na mashimo pamoja na kupita upande mmoja wa barabara kutokana uchakavu wa upande wa pili.

No comments:

Post a Comment