Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, June 2, 2010

Sh trilioni 11 ndio bajeti yetu!


SERIKALI ya Tanzania imepanga kutumia Sh trilioni 11.1 katika bajeti yake ya mwaka ujao wa fedha.

Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo jana aliiambia Kamati ya Bunge ya Fedha, kwamba katika mwaka 2010/11, Serikali imeongeza Sh trilioni 1.6 ikilinganishwa na mwaka jana wa fedha.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkulo alisema kati ya fedha hizo, zinazotarajiwa kukusanywa ni Sh trilioni 6 ambazo ni za mapato ya ndani na Sh trilioni 2.8 misaada na mikopo kutoka kwa wahisani.

Alisema pia kati ya fedha hizo, Sh trilioni 1.1 ni mikopo ya ndani, Sh bilioni 983.7 mikopo ya masharti ya kibiashara na Sh bilioni 30 ni mapato kutokana na ubinafsishaji.

Waziri aliongeza kuwa vipaumbele katika bajeti hiyo vitakuwa ni katika kilimo, huduma za jamii kama elimu, afya na maji, ardhi na umwagiliaji, miundombinu ambayo ni reli, bandari, viwanja vya ndege na nishati.

“Hata hivyo, Serikali itatoa umuhimu wa kipekee katika bajeti yake ya mwaka 2010/11 kwa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu, ili kuhakikisha unafanyika kama ilivyopangwa na mradi wa vitambulisho vya Taifa kutokana na umuhimu wake kiuchumi na kijamii,” alisema Mkulo.

Kulingana na kiasi hicho kinachotarajiwa kupatikana katika bajeti hiyo, alisema Serikali inatarajiwa kutumia Sh trilioni 7.8 kwa matumizi ya kawaida na Sh trilioni 3.2 kwa matumizi ya maendeleo.

No comments:

Post a Comment