Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Sunday, June 13, 2010

England yabanwa na watoto wa Obama!!



Mechi kati ya ENGLAND na USA iliyofanyika katika kiwanja cha Rustenburg - Royal Bafokeng Stadium.

Haikuweza kuzaa matunda kwa Waingereza ambao toka awali walionekana wamepania sana na kujiandaa vyema katika mechi hiyo na huku asilimia kubwa ya mashabiki na wapenzi wa soka wa timu hiyo walikuwa na mategemeo makubwa na timu hiyo,baada ya kushindwa kuzitumia nafasi vyema ambazo zingeweza kuzaa matunda na kujikuta wakipoteza nafasi hizo.

Na hatimaye ENGLAND wakijikuta wakitoka sare ya goli 1-1 na USA, Goli hilo kwa upande wa ENGLAND lilifungwa na mchezaji STEVEN GERRARD mnamo dakika ya 4 na kwa upande wa USA waliweza kurudisha bao hilo lililofungwa na mchezaji CLINT DEMPSEY mnamo dakika ya 40.

Na katika mechi hiyo mchezaji TIM HOWARD alichaguliwa kuwa MAN OF THE MATCH.

No comments:

Post a Comment