Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Saturday, April 24, 2010

MOTO WAZUA KIZAAZAA BENKI YA NMB TAWI LA BANK HOUSE!!


Moshi uliozusha hofu kwa wateja na wafanyakazi wa banki ya NMB tawi la Bank House lililopo mtaa wa Samora, baada ya moto kulipuka katika benki hiyo , haikufahamika mara moja chanzo cha moto lakini upande uliolipuka moto ndiyo eneo lililokuwa likitumika mwanzo na benki hiyo kutoa huduma kwa wateja, hivi karibuni upande huo ulifungwa na wateja walihamiswa na kuendelea kupata huduma ghorofa ya tatu.
Upande huo unafanyiwa ukarabati na mafundi kitu ambacho kinasadikiwa kuwa huenda ndiyo chanzo cha moto huo katika benki hiyo, nilikuwepo katika benki hiyo nikipata huduma na nilipomaliza nilishuka chini, nilipofika kwa walinzi wa benki hiyo nikasikia wakisema kuna moto unawaka, mara nikasikia king'ora kikilia.
Walinzi walitoa taarifa kwa uongozi ndipo watu wakaaza kukimbia hovyo huku moshi ukiendelea kusaambaa katika jengo hilo, hata hivyo wafanyakazi wa kampuni inayofanya kazi ya kukarabati jengo hilo walijaribu kuudhibiti moto huo na kufanikiwa kwa kiasi fulani kabla ya kikosi cha Zimamoto waliokuwa wamechelewa sana kufika eneo la tukio na kuchukua hatua za kuuzima

No comments:

Post a Comment