Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, April 23, 2010

MAJAMBAZI SUGU 18 MBARONI!!!


Kamanda wa Kanda maalum ya Dar es Salaam Suleiman H. Kova akionyesha waaandishi wa habari Ofisini kwake leo Silaha zilizokamatwa na jeshi la polisi kwa msako maalum pamoja na kutaja orodha ya majambazi yaliyotiwa nguvuni na jeshi la polisi.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limefanikiwa kuwakamata majambazi sugu 18 , kufuatia uchunguzi wa kikachelo wa muda mrefu kwa makosa ya mauaji, unyang’anyi wa kutumia silaha,ubakaji, uvunjaji wa migahawa na wizi wa kutumia nguvu.

Akizungumza na waandishi wa Habari mapema ya jana asubuhi Kamanda wa jeshi hilo, Suleimani Kova alisema kati ya majambazi hao watano walikamatwa na silaha 3 ambazo ni bastola 2 na bunduki moja iliyotengenezwa kienyeji.

Bastola zilizokamatwa ni aina ya CESCA yenye NO.127159 iliyokuwa na risasi 4. nay a pili ilikuwa aina ya Chinese Pistol yenye NO. N001292 yenye risasi mbili.Pia bunduki iliyotengemnezwa kienyeji (Home made Gun) gobore iliyokutwa imeshindiliwa tayali kwa matumizi.

Kova aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni; Abdul Hamis Kinyunguza ambaye alikutwa na bastola aina ya CESCA. Ambaye ni mkazi wa Buza kanisani.

Said Athumani alikutwa na na Bastola aina ya CHINESE, ambaye ni mkazi wa Tanga mtaa wa maandazi, kwa upande wake Omari Abdul na wengineo walikutwa kwa makosa mbalimbali ya kujihusisha na uhalifu

Katika tukio la kujeruhi ambalo nilakusikitisha lililotokea jana tarehe 21.4.2010 majira ya saa 10 na dakika 50 jioni huko maeneo ya Mbagala Kingugi (W) Temeke Mtoto wa Kiume aliyetambulika kwa jina la Denatus Deminikus(4) mkazi wa Mbagala Kingungi aliyejeruhiwa kwa kuunguzwa na uji wa moto sehemu zake za siri na mapajani na shangazi yake aliyefahamika kwa jina la Bi.Deminata Theonest(29) mkazi wa Mbagala Kingugi ambaye ndiye alikuwa akiishi naye,Sababu ya kumuunguza motto huyo bado hajafahamika.Majeruhi amelazwa hospitali ya Temeke,Shangazi huyo alimchukua motto huyo toka Bukoba na kuja naye DSM kwa ajili ya kumlea na matokeo yake amekuwa akimfanyia vitendo vya ukatili Mtuhumiwa amekamatwa na upelelezi unaendelea,alisema Kamanda Kova.

No comments:

Post a Comment