Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Tuesday, April 27, 2010

Omar Al Bashir Kutangazwa mshindi??


Matokeo ya kwanza kufuatia uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi katika kipindi cha miaka 24 yanatazamiwa kutangazwa leo nchini Sudan.
Mwandishi wa BBC mjini Khartoum anasema Rais Omar al Bashir anatazamiwa kutangazwa mshindi.
Salva Kiir, aliyekuwa kiongozi wa waasi wa kusini, SPLM, ametangazwa mshindi, kama rais wa serikali ya kusini, ambayo kwa kiasi fulani ina madaraka ya uongozi.

Uchaguzi katika sehemu zote ulikuwa na malalamiko mengi ya udanganyifu, na pia vitisho kwa wagombea, huku wasimamizi wa kimataifa nao wakisema kwamba viwango vya uchaguzi huo kamwe havikubaliki.

No comments:

Post a Comment