Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, April 30, 2010

Wahadhiri UDSM waanza mgomo!



Wakufunzi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wameanza mgomo wa kutoingia madarasani kufundisha ili kuishinikiza Serikali kuwalipa na kuboresha mafao yao ya kazi.
Akielezea uamuzi huo kwa vyombo vya Habari leo, Mwenyekiti wa Umoja wa Wahadhiri chuoni hapo Damas Nyaoro amesema kimsingi Wahadhiri wastaafu wanataabika kwa kutolipwa mafao yao kwa muda mrefu na wengine kupewa malipo madogo yasiyolingana na vigezo vya taaluma.

Amesema suala hilo la kuboreshewa mafao yao limekuwa likilalamikiwa kwa muda mrefu na Serikali haijachukua hatua yoyote jambo linalozidi kuzorotesha hali ya Wahadhiri hao kimaisha.

Hatua hiyo ya Wahadhiri UDSM imechukuliwa katika wakati ambao Serikali inahaha kuzima mgomo mkuu wa Wafanyakazi wote ulioitishwa kufanyika siku chache zijazo mwanzoni mwa mwezi ujao.

No comments:

Post a Comment