Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, April 28, 2010

Niliowamwaga Kundini Ni Wavivu!


King wa Miondoko ya Kwaito Bongo, Juma Kassim Kiroboto a.k.a Nature ambaye juzikati aliwapa shiti washkaji zake waliokuwa wakiunda Crew ya Wanaume TMK Halisi, amewadisi jamaa hao aliowaacha yatima baada ya kula mkataba na Kampuni ya DLC ya nchini China.
Nature aliwachana jamaa hao alipokuwa akigonga interview na stesheni moja ya redio jijini Dar mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo mtu mzima alieleza chanzo cha kuwatosa kwenye shavu hilo.
“Tumewaacha kwa sababu ni wavivu wa kuandika na pia tulijua mwishoni watajiondoa wenyewe kundini. TMK Halisi hii mpya ni kazi kwa kwenda mbele, hatutaki tena watuma meseji,” alisema Nature bila kufafanua ni meseji za aina gani.

Wasanii wanaoendelea kuwakilisha TMK Halisi na Nature ni pamoja na Dolo, Baba Levo, JB wa Mabaga Fresh na KG Son. Waliotoswa ni Luteni Kalama, Mzimu, Malipo, D Chief, Bob Q, BK na Richie One ambaye alikuwa ni mshkaji wa karibu wa Nature.

No comments:

Post a Comment