Habari mbalimbali toka pande za bongo bila kusahau matukio mbalimbali yanayorindima pande zote za dunia
Psquare Ft. J.Martins- E No Easy
Saturday, April 10, 2010
LIYUMBA AFUTIWA SHITAKA
Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba aliyekuwa akikabiliwa na mashitaka mawili, kutumia vibaya madaraka na kuisababishia serikali hasara ya Shilingi bilioni 221 leo ameondolewa shitaka la kutumia vibaya madaraka na hivyo kubaki na kosa moja.
Liyumba aliyekuwa akikabiliwa na kesi hiyo Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, alifutiwa shitaka hilo baada ya mawakili wa upande wa utetezi kutoa vielelezo vilivyothibitisha kuwa mteja wao hakuwa na kesi ya kujibu.
Mshitakiwa huyo amerudishwa Keko mpaka Aprili 22 mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment