Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, April 23, 2010

Kimwana Manywele msagaji?


Kimwana Manywele namba (2) 2006-07, Husna Idd ‘Sajent’ hivi karibuni aliwashangaza wageni waalikwa katika sherehe ya kuzaliwa kwa Malkia wa Ngwasuma, Ketula Kihongosi pale alipowaacha watu wakisherehekea pati hiyo na kushughulika na vitendo vya kisagaji kwenye mwili wa mlengwa.

Kimwana huyo alionekana akichezea matiti ya mwenzake sambamba na kulishana keki kwa kutumia mdomo hadharani kitendo kilichowashtua wageni hao na kubaki wakijiuliza kulikoni Kimwana Manywele amekuwa na tabia za kisagaji?

Pamoja na watu kufurika katika sherehe hiyo iliyokuwa maalum kwa ajili ya kumpongeza malkia kwa kutimiza miaka kadhaa, Husna hakuwaogopa, alichukua muda mwingi kukaa karibu na aliyekuwa akisherehekewa na kuanza kumpapasa papasa na kumfanyia vitendo vya kisagaji huku picha zikichukuliwa na wanawake wengine wakimshangaa.

“Hivi kimwana siku hizi amekuwa msagaji? Ona anavyochezea kifua cha mwenzake, angalia alivyoshika matiti kama vile anamchezea mpenzi wake, huu si usagaji jamani?” Alisikika dada mmoja ambaye naye alikuwa ni miongoni mwa wageni waalikwa.

Aidha, kitendo cha Husna ‘Sajenti’ kuchukua muda mrefu na kutawala kwenye sherehe hiyo akionesha mapenzi makubwa kwa msichana mwenzake, kiliwashangaza wengi wakiwemo akina kaka waliokuwa karibu na malkia huku wakihoji kulikoni.

“Huenda hawa mabinti ni wasagaji, kwanini kila kona Sajent anakaa na malkia na hampi nafasi ya kuchati na wageni wengine… angalia kila mara anampiga mabusu,mh emu ninyamaze miye mambo haya ya mjini zaidi,” alisema kaka mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Issa.
Hata hivyo, mara baada ya sherehe hizo na wageni waalikwa wote kuondoka ‘Sajent’ alibaki ameganda hali iliyomfanya mwandishi wetu kumhoji.

Alipoulizwa sababu ya kutoondoka na kwanini alikuwa akifanya naye mambo yaliyotafsiriwa na watu kuwa ni ya kisagaji alijibu: “Hiki ndiyo kinakushangaza? Huyu ni rafiki yangu wa karibu sana hayo mambo ya kisagaji mimi sina na wala sijawahi kufikiria, ni tabia ambayo siipendi kabisa.
CHANZO GLOBALPUBLISHERS

6 comments: