Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Monday, April 26, 2010

Dominic Mwita Hatunaye Tena!


Hayati Dominic Mwita.

Chumba cha habari cha Daily News na HabariLeo kimeghubikwa na majonzi kufuatia habari ya kifo cha Dominic Mwita (32), aliyewahi kuwa mwandishi wa habari kwenye makampuni hayo kabla ya kuhamia kitengo cha habari cha UNICEF jijini Dar.

Kifo chake kimesababishwa na ajali ya barabarani siku ya Ijumaa usiku wakati marehemu aliyekuwa anatoka harusini na gari yake aina ya RAV4 aliingia kwa nyuma semi-trela lenye namba T632 AGH lililokuwa limesimamishwa katikati ya barabara kiasi cha mita 100 hivi toka daraja la Mbezi Beach jijini Dar.

Kamanda wa polisi wa Kinondoni Elias Kalinga amethibitisha kutokea ajali hiyo na kusema uchunguzi unaendelea. Aliongezea kusema tela hilo lilisimamishwa katikati ya barabara bila wenyewe kuweka tahadhari ya traiengo ama ala ingine kwa watumia barabara wengine.

Msiba uko nyumbani kwa shemeji wa marehemu, Bw. Fred Mwita, huko Mbezi Makonde ambako mipango yote ya mazishi inafanyika.

Marehemu Dominic, ambaye amewahi kufanya kazi Posta na Nyanza bottling huko Mwanza, amefanya kazi Daily News kati ya mwaka 2003 na 2005 kabla ya kuhamia UNICEF.

Mola aiweke mahala pema peponi roho ya marehemu

AMEN

Source www.issamichuzi.blogspot.com

2 comments:

  1. He was more than a friend I should say a brother. We were always hanging out together to an extent of many people thinking we were also together the day he had that fatal accident. We had alot of investment plans too for the great future of our families...

    He will always have a special place in our hearts because I believe if you got to know him then he must have touched your heart in one way or the other, he was gifted I guess....

    One precious memory you left us is our baby girl Dominica and her mother Angela. I promise to take care and support both of them as they were mine. By the way Dominica & my Brandy are blending up very close as they both grow up. Just like their fathers....

    Look up to us from heaven above and keep praying for us to always walk on the road of lightousness and finally meet again in the never ending heaven.

    You will always be missed, ofcourse tears go down whenever I remember you...MISS YOU BROTHER!!.

    Frankie Fransis

    ReplyDelete
  2. find more r6v37y4p17 replica louis vuitton replica bags philippines wholesale Check This Out u8m53u7v29 best replica bags online replica chanel bags ebay replica bags 168 mall replica hermes handbags w8n14u5r86 replica bags joy

    ReplyDelete