Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Monday, March 22, 2010

HAKUNA HELA MBOVU, ATAYEIKATAA KUSHITAKIWA!!



Serikali imewasihi na kuwaomba radhi baadhi ya wananchi kuacha kukataa baadhi ya fedha halali zilizoko kwenye mzunguko kwa madai kuwa hazifai kwasababu ya uchakavu wake.
Kwa mujibu wa katibu mkuu wa wizara ya uchumi na fedha, Ramadhani Kijah, hakuna sheria inayomruhusu mwananchi kuzikataa fedha hizo.
Alisema ingawa kuna malalamiko ya uchakavu wa koini za sh 100, alisema hiyo siyo sababu ya kuzikataa kwani zinatambulika na sheria.
"Fedha hizo zitumike hadi hapo zitapofika benki amabako ndiko zitakuwa mwisho wake kwani kule kuna watu maalumu waliojariwa kuteketeza pesa mbovu na hata hela chafu," alisema Kijah.
Kijah alisema kwa yeyote atakayepinga kupokea fedha hizo basi atambue kuwa anapingana na sheria zilizowekwa na serikali hivyo atakuwa anajijengea mazingira ya kufikishwa katika vyombo vya sheria.

No comments:

Post a Comment