Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Monday, March 22, 2010

UBALOZI WA NIGERIA NCHINI LIBYA WAFUNGWA SABABU YA GHADAFI!

Nigeria imemwamuru balozi wake nchini Libya, arejee nyumbani kufuatia matamshi ya rais Muammar Gaddafi, aliyopendekeza taifa hilo ligawanywe mara mbili, moja ya wakristo na nyingine ya waislamu.

Wizara ya mambo ya nje ya Nigeria imetaja matamshi hayo ya Gadaffi, kama ya uchochezi. Rais wa bunge la senate nchini Nigeria, David Mark amesema, rais Gadaffi ni mtu asiyekuwa na akili timamu.

Mapema wiki hii kiongozi huyo wa Libya, alisema njia ya pekee ya kusitisha mauaji ya raia nchini Nigeria ni kuigawa nchi hiyo kuwa mataifa mawili.

Mamia ya watu wameuawa katika siku za hivi karibuni nchini Nigeria kufuatia ghasia za kidini na kikabila katika jimbo la Plateau kati kati mwa nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment