Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, March 31, 2010

Khaaa!! Yule Mbwa aliyeibiwa si huyu hapa!!


Hapa ni mitaa ya Block 41 nyuma ya Best bite, kama unavyoona mbwa kabebwa na mshkaji. Hazijapita siku nyingi, mdau alitangaza kuibiwa mbwa wake mitaa ya sinza, mbwa mwenyewe ni huyu hapa. Mshkaji alikuwa anamuuza kwa sh elfu arobaini na tano.
Jamani mbwa kafundishwa kwa miaka kadhaa, halfu nasikia alikuwa mkali kupindukia lakini mshikaji akapita nae! Sasa kwa wale wenye mabull dog wanaouzwa sh millioni moja, kazi kwenu, wabongo hawachagui wala hawabagui. wabongo wameshindikana!!!

1 comment: