Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Wednesday, March 17, 2010

MIA TANO TU YA KITANZANIA YATAKA KUMTOA MTU ROHO!



Watoto mitaani wamekutwa na kamera yetu majira ya saa mbili leo asubuhi,nje ya jengo la PPF TOWER ambapo watoto hawa huzagaa chini ya jengo hilo nakuomba misaada kwa wapita njia.Watoto hawa ambao majina yao hayakuweza kupatikana mara moja wakiwa katika vuta nikuvute ya kugombania Tsh 500/= waliyopewa na mmoja ya wapita njia.



Mzozo hakuishia hapo………..watoto hawa wakionekana kuendelea kupokonyana jero hilo.


Ugomvi huo ukiendelea ambapo aliyekabidhiowa pesa hiyo kama anavyoonekana pichani akijaribu kujinasua mikono mwa wenzake,ambapo baada ya kuona kamera yetu waliamua kutawanyika kuogopa kupigwa picha.(Picha na INNO LYIMO)UMBEA BLOG.

No comments:

Post a Comment