Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Monday, March 1, 2010

Habari zilonifikia hivi punde! JUU YA AJALI YA NDEGE YA AIR TANZANIA



PICHA ZOTE ZIKIONYESHA NDEGE HIYO ILIVYOKUWA
Habari kutoka Mwanza zinasema kuwa ndege aina ya Boeing 737 ya Shirika la Ndege Tanzania imepasuka matairi mawili ya mbele na kusababisha kizaaa kikubwa kwa abiria wapatao 36 na wafanyakazi 7 waliokuwamo ndani ya ndege hiyo, mapema leo asubuhi. Hali hiyo ilitokea wakati ndege hiyo ikijaribu kutua huku hali ya hewa ikiwa mbaya kutokana na mvua kubwa inayoendelea kunyesha karibu nchi nzima. Inaelezwa kuwa baada ya matariri ya mbele kupasuka, ndege ilitembelea tumbo kwa mita kadhaa kabla ya kufanikiwa kusimama na abiria pamoja na wafanyakazi wake kutoka salama. Safari za ndege kubwa zimesimamishwa kwa muda uwanjani hapo.
Picha zote na mwandishi wetu jijini mwanza kader adara!

2 comments:

  1. duu hii kali, sasa hizo wheels zimepasuka kwanini?. zimechoka au kulikua na kitu kimetoboa, coz i know mvua pekeyake is not the reason kwa taili mbili za ndege kupasuka,,, good news bra!! lete more..
    Dee peter

    ReplyDelete