Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Thursday, March 4, 2010

AMA KWELI POMBE SIO CHAI!


Kamera yetu imekuta kituko hiki jana majira ya saa 10:00 usiku katika kituo cha mabasi cha Palm beach hotel karibu na daraja la manyoya ambapo kijana huyu alikuwa amepanda basi la Kivukoni kuelekea Mwananyamala,alipokuwa ndani ya basi hilo alikuwa akifanya fujo kutokana na kulewa kupita kiasi ndipo dereva pamoja na kondakta wa basi hilo kuamua kumshusha katika kituo cha mabasi cha palm beach karibu kabisa na tukio la manyoya ili kuondoa kero kwa abiria wengine waliokuwa kwenye basi hilo.




Askari polisi wa kituo cha Salender wakijiandaa kumbeba kijana huyo na kumpeleka hospitalini akiwa hajitambui,UMBEA.COM haikuweza kupata jina la kijana huyo.


Kama kuna mtu yoyote anamfahamu kijana huyu aidha ni ndugu wa kijana huyu aende katika kituo cha polisi cha daraja la Salender atapata taarifa za ndugu yake alipo!

No comments:

Post a Comment