Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Monday, May 24, 2010

Eritrea yalambishwa Bao 8-1 na Twiga Stars


Timu ya Wanawake ya Twiga Stars imeibuka kidedea baada ya kuichapa Timu ya Wanawake ya Eritrea bao 8-1 katika mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam. Mechi hiyo ilikuwa ni kivutio sana kutokana na kwamba haijawahi kutokea hapa nchini kwa Timu ya Wanawake kuweza kufungua mabao mengi kama ya leo.

Twiga Stars imefainikiwa kuvuka kipenga hicho na kujiwekea nafasi ya kwenda Bondeni Afrika ya Kusini kwa Mzee Madiba kushiriki mashindano ya nusu fainali za kombe la dunia kwa mataifa ya Afrika endapo tu watafanikiwa kulitetea taji hilo katika mechi ya marudiano na Timu ya Eritrea.

No comments:

Post a Comment