Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Sunday, May 23, 2010

Makamba akana kuingilia sakata la UV CCM!


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Yusuf Rajabu Makamba, amepinga vikali kuhusika katika kumlazimisha kujiuzulu aliyekuwa Mwenyekiti Umoja wa Vijana wa CCM Taifa Hamad Massauni, na kusema Masauni aliwajibika mwenyewe.
Makamba amesema baada ya kupata uvumi kuwa mwenyekiti huyo aligombea uongozi akiwa hana vigezo kutokana na umri wake kuzidi, walifanya uchunguzi na kuthibitisha kuwa tayari alishatimiza miaka 35 wakati anagombea.

Amesema alichokifanya ni kujadiliana naye tu kuhusu suala hilo na kwamba hakumlazimisha kujiuzulu.
Mimi nilimwambia kama umekosa kalale, ufikirie na upime mwenyewe kwa kosa hilo; na asubuhi akarudi na kusema nimejiuzulu, ameeleza Makamba.
Taarifa hiyo imekuja baada ya wadau wengi kumhusisha Makamba na sakata hilo kwa kudai kuwa alimshinikiza kiongozi huyo wa vijana kuachia ngazi.

No comments:

Post a Comment