Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Thursday, May 27, 2010

K’sher akacha camera za mapaparazzi Club!!


Msanii peke wa kike toka kundi la Tip Top Connection Khadija Shaaban a.k.a K'sher amedai kitendo cha kukataa kupigwa picha na paparazi siku za hivi karibuni bila ridhaa yake ni uamuzi wake mwenyewe. K'Sher aliyasema hayo baada ya mvutano uliotokea wiki chache za nyuma baina yake na wapiga picha wa magazeti tofauti nchini katika Club ya Sansiro iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.

K’Sher aliyasema hayo baada ya mvutano uliotokea wiki chache za nyuma baina yake na wapiga picha wa magazeti tofauti nchini katika Club ya Sansiro iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.

“Unajuwa unapotoka usiku huwa unavaa mavazi ya usiku zaidi ukiwa unaenda sehemu kama club, sasa siku ile pale Sun Cirro nilikuwa nimevaa aina hiyo ya mavazi ya Club na sikupendezwa kuonekana katika hali ile mbele ya jamii kwani haipendezi” alisema K’Sher

Zaidi aliongeza “Mimi ni kioo cha jamii, ninapopigwa picha nikiwa na mavazi ya Club sidhani kama ni maadili kwa picha hizo kusambaa magazetini kwani nipo katika sehemu ya burudani yangu na si kwa ajili ya kupigwa picha” alisema K’Sher

“Najua wapo kazini, wanaponipiga picha nikiwa jukwaani sikatai lakini katika sehemu za burudani ya mtu binafsi wanamvurugia mtu uhuru wake na si vema hata kidogo” alimaliza.

No comments:

Post a Comment