Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Monday, May 24, 2010

Jamani, Maunda Zorro si Ulee mtoto kwanza!!


Huku kichanga chake kikiwa na takribani miezi mitatu tangu kilipoingia duniani, Bongo fleva Diva, Maunda Zorro, amezua viulizo na kutoa ‘chansi’ kwa wadau wa burudani nchini kumpa ushauri wa bure wakimtaka atulie nyumbani na kulea mtoto.
Jamaa hao walifikia hatua hiyo baada ya Maunda kuonekana akijirusha ile mbaya ndani ya klabu kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar wiki iliyopita kwenye ‘afta pati’ ya tuzo za Kili.
Wadau hao waliamua kumtolea uvivu walidai kwamba, ni mapema mno kwa Maunda kujiachia na kwamba mtoto alimwachia nani hivyo kumtaka atulie nyumbani ili kulea mtoto hadi atakapofikia ‘eji’ ya kufanya hivyo.

“Hebu muone Maunda anavyojiachia, mtoto atakuwa amemwachia nani? Maunda anatakiwa atulie nyumbani alee mtoto hadi akiwa na umri wa kumwacha ndiyo afanye haya anayoyafanya,” alisema mmoja wa wadau hao.

No comments:

Post a Comment