Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Saturday, May 22, 2010

Hukumu ya Liyumba Kusomwa Jumatatu!


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam itatoa hukumu ya kesi inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala Benki Kuu Tanzania (BoT), Amatus Liyumba siku ya jumatatu tarehe 24.
Liyumba kwa sasa anakabiliwa na shitaka moja la kudaiwa kutumia vibaya ofisi ya umma. Awali alishitakiwa pia kwa kudaiwa kuisababisha hasara ya Sh bilioni 221,upande wa mashitaka ulishindwa kudhibitisha shitaka hilo, likafutwa.

Liyumba alidai kuwa yeye hakuwa na mamlaka ya kuidhinisha mradi huo na kwamba, aliyekuwa Gavana kwa wakati huo, Daudi Ballali, ndiye aliyekuwa na mamlaka yote.
Katika ushahidi huo, Liyumba pia ameieleza mahakama kuwa,ingawa mradi huo ulikuwa chini ya kurugenzi yake, hakuwa anahusika kushughulika na mradi huo ingawa mara kadhaa alijibu barua zinazohusiana na mradi kwa maelekezo ya Gavana.

No comments:

Post a Comment