Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Saturday, May 22, 2010

Mama Salma ashiriki katika Mjadala wa wanawake-Beijing!




Mke wa Rais Mama Salma Kikwete alihutubia mkutano wa wanawake wa dunia katika kuelezea mafanikio aliyoyapata katika taasisi yake ya wanawake na maendeleo (WAMA) na juhudi zake binafsi za kusaidia ugonjwa wa saratani ya shingo ya kizazi.
Mama Kikwete ambae ametajwa kuwa mfano bora kwa wake wa marais wa Afrika kufuatia taasisi yake ya WAMA kujikita zaidi katika kusaidia jamii na hasa jitihada zake binafsi za kusaidia wanawake,afya, na watoto wanaoishio katika mazingira hatarishi.
Akijibu maswali kwa kujiamini , Mama Kikwete Kiwete alisema madhumuni makubwa ya kuanzishwa kwa WAMA ni kumuendeleza mwanamke kielimu, kiafya na kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi na wale wanaishi katika mazingira hatarishi.

Alisema kuwa vitu vingi amekuwa akifanya kupitia taasisi yake ya WAMA kusaidia wanawake wa Kitanzania ikiwemo suala la elimu kwa kuwa ndiyo njia pekee ambayo inaweza kumkwamua mwanamke katika maisha ya chini na hili amekuwa ameanza kwa wasichana wadogo kuwasisitiza umuhimu wa elimu na kujiepusha na mimba za utotoni na hususan swala la kujiepusha na ugongwa wa ukimwi.

No comments:

Post a Comment