Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Saturday, May 29, 2010

Wananchi wavamia polisi na kuua majambazi!


Mamia ya watu wakiwa na silaha wamevamia na kuvunja kituo cha kidogo cha polisi cha kata ya Mbarika, wilayani Misungwi kisha kuua watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi sugu.
Imeelezwa kuwa askari polisi wa kituo hicho, walizidiwa nguvu na wananchi hao, hali iliyosababisha kukimbia ili kuokoa maisha yao.

Habari za kuaminika kutoka eneo la tukio zinasema majambazi hayo yalikamatwa wakati yakijiandaa kufanya uhalifu na kufikishwa kituoni hapo kwa ajili ya kufikishwa mbele ya vyombo vya dola.

Habari zinasema, majambazi hayo yameuawa vibaya kwa kuchanwachanwa huku baadhi ya viungo vyao kama vile utumbo vikiwa vimezagaa katika eneo la tukio.

Imeelezwa katika tukio hilo, polisi walizidiwa nguvu kutokana na kituo hicho kutokuwa na silaha hata moja wala mabomu ya machozi.

No comments:

Post a Comment