Habari mbalimbali toka pande za bongo bila kusahau matukio mbalimbali yanayorindima pande zote za dunia
Psquare Ft. J.Martins- E No Easy
Monday, May 3, 2010
Obama atembelea eneo yanakovuja mafuta!!!
Rais Barack Obama wa Marekani ameelezea kuvuja kwa mafuta katika Ghuba ya Mexico ni janga kubwa la kimazingira ambalo halijawahi kutokea.
Akizungumza huko Louisiana, Bw Obama alisema serikali yake itafanya kila linalowezekana kuondoa mafuta hayo, na kuongeza kuwa BP inahusika na kuwajibika kwa gharama za usafishaji wa mazingira.
Alisema kazi ya muhimu kwa sasa ni kuzuia mafuta yasisambae zaidi katika pwani ya Ghuba.
BP inasema itachukua zaidi ya wiki moja kabla ya mipango ya dharura kuzuia uvujaji huo haijaanza kuzaa matunda.
Lakini huenda kazi ya kuchimba visima vya pembeni kusaidia kunyonya mafuta ikamalizika baada ya miezi kadhaa kumaliza kabisa tatizo hilo, Waziri wa mambo ya ndani, Ken Salazar alionya siku ya Jumapili.
Mtambo unaoendeshwa na BP wa kuchimbia mafuta ujulikanao kama Deepwater Horizon, ulizama tarehe 22 Aprili, siku mbili baada ya mlipuko kuua watu 11.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment