Psquare Ft. J.Martins- E No Easy

Friday, May 21, 2010

Njama ya Al Qaeda kufanya Ugaidi Kombe la Dunia Yafichuliwa!


Pichani ni Abdullah Azam Saleh al-Qahtani anayedaiwa kuwa mfuasi wa al-Qaeda aliyetiwa kizuizini Iraq ambapo ametoa maelezo juu ya mpango wa kutaka kufanya shambulio Kombe la Dunia Afrika Kusini mwezi ujao.
Mtu huyo raia wa Saudi Arabia, amewaambia waandishi wa habari alipanga kushambulia timu ya Uholanzi na Denmark kwa kulipiza kisasi baada ya kuchora vibonzo vya mtume Muhammad.
Lakini amesema viongozi waandamizi wa al-Qaeda bado hawakuidhinisha mpango huo.
Aliendelea kwa kusema "Kama tusingeweza kufikia timu zao, basi tungewalenga mashabiki wao."
Mpango huo ungehusisha mabomu ya magari na mashambulio kwa kutumia bunduki.

No comments:

Post a Comment